Sonzaschool
Rudi

Sekondari ya Juu · Kidato cha Tano

Kiswahili 1

Matawi ya sarufi

takriban dakika 9 kusoma

Mada za sehemu hiiMatumizi Ya SarufiMada 7

  1. Dhana ya sarufi ya lugha imefafanuliwa na wataalamu mbalimbali wa sarufi.

  2. Mtaalamu James Salehe Mdee (1999) anafafanua maana ya sarufi kuwa ni mfumo wa kanuni za lugha zinazomwezesha mzungumzaji kutunga sentensi sahihi na zenye kukubaliwa na wazawa wa lugha.

    • Kanuni hizi hujitokeza katika lugha ya mzawa wa lugha inayohusika ambaye anaifahamu barabara lugha yake.
    • Sarufi inajumuisha mfumo wa sauti, maumbo ya maneno, muundo, na maana.
  3. Mtaalamu Mbundo Msokile (1992) na Khamisi (1978) wanasema sarufi ni mfumo wa taratibu na kanuni zinazotawala matumizi sahihi ya:

    • Matamshi,
    • Maumbo ya maneno,
    • Miundo ya tungo,
    • Maanda ya miundo ya lugha.
    • Ni mfumo wa taratibu zinazomwezesha mzungumzaji wa lugha kutoa tungo sahihi.
    • Inamwezesha mtu yeyote anayezungumza kuelewa tungo zinazotolewa na mtu mwingine anayetuma lugha hiyo hiyo.
  4. Nkwera (1978) anasema sarufi ni utaratibu wa kanuni zinazomwezesha mzawa au mtumiaji yeyote wa lugha kuelewa tungo zinazotolewa na mtu mwingine anayetunza lugha hiyo hiyo.

    • Kufafanua na kuzielewa kwa undani tungo mbalimbali zitumikazo katika lugha hiyo pamoja na kutoa tungo sahihi na zinazoeleweka.

Mwalimu

Unasoma somo hili? Niulize nikuelezee chochote kilichomo.

Ingia ili kumuuliza Mwalimu wa AI wa Sonza kuhusu mada hii.

Ingia ili kuuliza