Sonzaschool
Rudi

Sekondari ya Juu · Kidato cha Tano

Kiswahili 1

Sentensi

takriban dakika 12 kusoma

Mada za sehemu hiiMatumizi Ya SarufiMada 7

Sentensi

  1. Sentensi ni kifungu cha maneno kinachoanzia neno moja na kuendelea lakini chenye muundo wa kiima na kiarifu au kikundi nomino na kikundi kitenzi.
  2. N.B: Sentensi ndiyo tungo kubwa kuliko tungo nyingine zote katika mpangilio wa tungo.

  1. Sentensi ina sehemu kuu mbili (2):
    • Sentensi ikigawanywa kwa kutumia kigezo cha kidhima ina sehemu kuu mbili ambazo ni KIIMA na KIARIFU.
    • Sentensi ikigawanywa kwa kuangalia muundo wa sentensi basi sentensi hugawanywa katika sehemu kuu mbili yaani KIKUNDI NOMINO na KIKUNDI KITENZI.
  2. Mgawanyo huu hutokana na kanuni kuu ya kisintaksia ambayo hudai kila sentensi iliyosahihi na inayokubaliwa na wazawa wa lugha ya Kiswahili ni lazima iwe na muundo wa kiima na kiarifu au kikundi nomino na kikundi kitenzi.
  3. Kiima hutaja mtenda au mtendwa wa jambo na kiarifu huarifu jambo linalotendwa na kiima au alilotendwa na kiima.
    • Mfano: Juma anacheza mpira. Juma ni kiima (mtendwa) na kiarifu ni anacheza mpira.
    • Hapa pia nomino mpira ndiyo kiima, lakini kiima hiki kinataja kile kinachotendwa, yaani mpira.

Mwalimu

Unasoma somo hili? Niulize nikuelezee chochote kilichomo.

Ingia ili kumuuliza Mwalimu wa AI wa Sonza kuhusu mada hii.

Ingia ili kuuliza