Mada za sehemu hiiKuonesha Uelewa Wa Jambo Ulilolisikiliza Au KulisomaMada 6
Hadithi ni masimulizi yenye kusimulia habari fulani. Ni masimulizi yanayotumia lugha ya mjazo au nathari na mtiririko wake huwa mwepesi au sahili. Zipo hadithi za kubuni na zingine za kihistoria.
Soma hadithi ifuatavo, kisha jibu maswali
Hapo zamani za kale Sungura na ngiri walikua marafiki wakubwa. Walikua wakitembea pamoja na kufanya shughuli zao pamoja. Siku moja walipanga kwenda safari ya mbali. Basi siku llipowadia, walifunga safari bila hata kuchukua chakula na fedha. Ngiri alimweleza rafiki yake hakuna haja ya kubeba chakula kwani chakula kingi kipo njiani. Hivyo asiwe na wasiwasi. Baada ya kutembea kitambo kidogo, ngiri alimwambia rafiki yake, "Iwapo utaanza kuona chochote kile kinacholiwa utakula peke yako".
Baada ya mwendo mfupi, Sungura akaona maembe, kabla ngiri hajayaona. Akamwambia ngiri, Nimeyaona maembe, hivyo nitakula peke yangu. Ngiri akamjibu maembe vale ni yangu mimi ndiye niliyeanza kuyaona ndio maana ninayachekelea. Au unajifanya hunioni ninavyoyachekelea? Sungura alistaajabu na kujisemea kimoyomoyo, "Meno ya ngiri wakati wote yako nje na si kwamba anacheka. Sasa iweje anadai eti anachekelea maembe?" Hata hivyo, kwa kuwa hakuwa na nguvu kama ngiri, alimwacha ale yale maembe. Alipomaliza waliendelea na safari mbele kidogo, Sungura aliona mapapai. Basi mara akamuuliza ngiri, "Je umeona chochote?" Kwa kuwa ngiri haoni mbali alijibu, "sijaona chochote. Kwani wewe umeona nini?" Hapo Sungura alipata faraja akamwambia ngiri nimeona mapapai hivyo nitakula peke yangu" ngiri aliposikia hivyo alisema kwa ukali, "Mapapai hayo ni ya kwangu, nami niliyaona tangu mbali ndiyo maana nilikua nayachekelea. Niliposema sijaona kitu nilikuwa nakudhihaki tu". Ngiri alikula mapapai vote peke yake. Sungura alipoona mambo yanazidi kuwa magumu, alichelea kufa kwa njaa kwani rafiki yake alikua anamdhulumu kila alichokiona. Sungura alijiona yupo kwenye ukingo wa kaburi kwani angeweza kufa wakati wowote kutokana na njaa.
Safari iliendelea lakini Sungura aliwaza namna ya kumtelekeza ngiri ili asife njaa. Mara walifika kwenye msonobari. Nyuma ya msonobari walimsikia simba akikoroma. Sungura alijisemea, "sasa wakati wangu wa kulipa kisasi umefika". Basi Sungura alianza kupiga kelele na kucheka ovyo. Ngiri alikua haelewi kwanini Sungura anafanya vile. Hatimae kicheko kilimwamsha simba. Simba aliuliza, "Nani anapiga kelele namna hii wakati mimi nimejipumzisha?" Ngiri alijibu, "Sungura ndiye anayecheka hovyo". Sungura alijibu kwa unyenyekevu, "Hapana si mimi, mfalme wangu mtukufu. Ngiri ndiye aliyekua anacheka hovyo, unamwona anaendelea kucheka?" ngiri alijitetea, "Haya ni maumbile yangu tu. Meno yangu yako nje wakati wote na sio nakucheka", Sungura alizidi kumkandamiza, "Anakudanganya huyo, mfalme. Mwangalie, hadi sasa meno yake bado yako nje, anaendelea kukucheka. Anasema eti una nywele mpaka machoni."
Ngiri alijitahidi kukataa na kujitetea lakini maneno yake hayakufua dafu mbele ya hasira za simba. Simba alimrukia na kumrarua, kisha akamla. Wakati simba aliposhiba, alilala usingizi mzito. Sungura alijizoazoa kwa tabu na njaa yake na kurudi nyumbani. Ama kweli shibe mwana malevya na njaa ni mwana malegeza
Wahusika katika hadithi ni watu na viumbe wa kubuni wanaotokea katika hadithi. Watu na viumbe hao hutumiwa kuwakilisha tabia za watu halisi katika jamii ili kutoa mafunzo au ujumbe.
Tabia za wahusika huonekana kupitia mambo wanayoyatenda na maneno wanayoyazungumza, mambo wanayoyapenda na yale wanayoyachukia. Mfano kuna wahusika wema na aliyekua akiishi mbali wavivu
Soma habari ifuatayo kisha jibu maswali
Wamasai ni kabila pekee lenye kutunza mila zao na desturi zao. Kabila hili ni maarufu kwa shughuli za ufugaji. Wao huishi kwa kutegemea wanyama. Wamasai hujulikana kirahisi kutokana na utamaduni wao kuwa wa kipekee. Vazi lao la rubega na utoboaji wa masikio pia uvaaji shanga mkononi na miguuni ni alama zinazotambulisha wamasai.
Wamasai huishi kwa kuhamahama kwa ajili ya kutafuta malisho kwa ajili ya mifugo yao. Ufugaji wa kimasai ni wa kizamani kwani hufuga idadi kubwa ya mifugo. Ufugaji wa kisasa unalenga kufuga idadi ndogo ya mifugo kwa njia za kitaalamu.
Mifugo ifugwayo na wamasai ni ile yenye kustahimili uhamiaji. Mifugo hiyo ni kama ng'ombe, mbuzi, kondoo na punda. Wanyama hawa huwapatia maziwa, nyama, ngozi na pesa wauzwapo. Punda huwasaidia kubeba mizigo. Wamasai pia hufuga mbwa kwa ajili ya ulinzi.
Wamasai hutumia akili zao na muda wao mwingi kulinda mifugo yao dhidi ya maadui. Kundi maalumu la vijana wa kimasai liitwalo morani hulinda mifugo. Wanyama waishio porini kama simba, chui, fisi na nyoka ni hatari kwa mifugo yao. Hivyo wamasai hubeba silaha za kiulinzi ili kukabiliana na wanyama hao wa porini.
Mwalimu
Unasoma somo hili? Niulize nikuelezee chochote kilichomo.
Ingia ili kumuuliza Mwalimu wa AI wa Sonza kuhusu mada hii.
Ingia ili kuuliza