Sonzaschool
Rudi

Msingi · Darasa la Sita

Kiswahili

Kubaini hoja Katika Majadiliano

takriban dakika 1 kusoma

Mada za sehemu hiiKuonesha Uelewa Wa Jambo Ulilolisikiliza Au KulisomaMada 6

MAZOEZI YA LUGHA

Kanusha sentensi zifuatazo

  1. Fundi huyu ameshona nguo zangu vibaya Fundi huyu hajashona nguo zangu vibaya

  2. Kiranja amewahi shuleni Kiranja hajawahi shuleni

  3. Kiatu hiki ni kipya Kiatu hiki si kipya

  4. Shule ina upungufu wa samani Shule haina upungufu wa samani

  5. Shambani kwetu ni mbali na mjini Shambani kwetu si mbali na mjini

  6. Kutembea gizani ni kuzuri Kutembea gizani si kuzuri

  7. Shule yetu ina maktaba kubwa Shule yetu haina maktaba kubwa

  8. Huyu ni daktari bingwa Huyu si daktari bingwa

  9. Kazi ya kulima ina changamoto kubwa Kazi ya kulima haina changamoto kubwa

  10. Mwajuma ni mtoro Mwajuma si mtoro

  11. Mtoto mkorofi hupendwa na mwalimu Mtoto mkorofi hapendwi na mwalimu

  12. Salumu aliishia darasa la sita Salumu hakuishia darasa la sita

  13. Rushwa huwaathiri watu wenye fedha tuu Rushwa haiwaathiri watu wenye fedha tuu

  14. Kwetu kuna milima mingi Kwetu hakuna milima mingi

Mwalimu

Unasoma somo hili? Niulize nikuelezee chochote kilichomo.

Ingia ili kumuuliza Mwalimu wa AI wa Sonza kuhusu mada hii.

Ingia ili kuuliza