Mada za sehemu hiiMatumizi Ya LughaMada 5
- Rejesta
- Misimu
- Umahiri wa lugha
- Utata katika matumizi ya lugha
- Utumizi wa lugha
Utumizi wa Lugha
-
Matumizi ya lugha ni namna ya kutumia lugha kulingana na mila, desturi na taratibu zilizopo katika jamii husika.
-
Ni jinsi ambavyo mzungumzaji anatunza lugha kwa kuzingatia uhusiano wake na yule anayezungumza naye.
-
Matumizi ya lugha hutegemea mambo kadhaa kama vile:
- Uhusiano baina ya wazungumzaji
- Mada inayozungumzwa
- Mazingira waliyemo wazungumzaji n.k
Umuhimu wa matumizi ya lugha
- Kuwasaidia watumiaji wa lugha kutumia lugha kwa ufasaha
- Kumsadia mzungumzaji kuweza kutambua kutofautiana na kutumia mitindo mbalimbali ya lugha
Mtindo wa lugha
- Mtindo wa lugha ni mabadiliko yanayojitokeza katika kutumia lugha, mabadiliko ya lugha katika mitindo mbalimbali yaani mitindo mbalimbali ya lugha.
- Kwa kawaida mtindo wa lugha / mabadiliko katika kutumia lugha ndiyo inayomwongoza mzungumzaji katika kuelewa maneno na mitindo ya tungo.
Matumizi katika lugha hutawaliwa na mambo yafuatayo:
- Uhusiano baina ya wazungumzaji
- Mada ya mazungumzo
- Lengo au madhumuni ya mazungumzo
- Sifa za wazungumzaji
- Jinsi mazungumzo yanavyofanywa
- Utanzu wa mawasiliano
Mazingira / Muktadha
- Ni wazi kwamba wazungumzaji huzungumza wakiwa katika mazingira fulani yanayotawala katika maisha yao ya kila siku.
- Mazingira hayo yanaweza yakawa ya hotelini, shuleni, ofisini, mahakamani na n.k
Uhusiano baina ya wahusika
-
Uhusiano baina ya wahusika huathiri mtindo wa uzungumzaji katika lugha.
-
Mzungumzaji atatumia lugha kwa kutegemea anaongea na nani, na kutokana na sababu hiyo tunapata:
- Lugha ya baba na mtoto
- Watu wa rika moja
- Mtu na mpenzi wake
- Mtu na mwanafunzi wake
- Mfanyakazi wa kawaida na mkuu wake wa kazi n.k
Mada ya mazungumzo
-
Kimsingi mada ya mazungumzo hutawala usemaji na namna ya uzungumzaji kwa ujumla
-
Kutokana na mada ya mazungumzo tunapata lugha ya:
- Kibiashara
- Kitaalamu
- Kitabibu
- Kitaaluma
- Kisiasa n.k
Madhumuni ya mazungumzo
-
Wakati mwingine mitindo wa lugha hutawaliwa na madhumuni ya mazungumzo
-
Kutokana na madhumuni ya mazungumzo, uzungumzaji utategemea:
- Mazingira
- Uhusiano baina ya wahusika
- Mada ya mazungumzo
Jinsi mazungumzo / mawasiliano yanavyozungumzwa
-
Namna mawasiliano yanavyofanyiwa inaweza kuathiri mtindo wa uzungumzaji
-
Mawasiliano yanaweza kufanywa kwa njia ya:
- Maandishi
- Mazungumzo ya mdomo
- Simu
- Televisheni
- Redio
-
Njia hizi huathiri mtindo wa uzungumzaji
Utanzu wa mawasiliano
-
Mtindo wa uzungumzaji unaweza kuathiriwa pia na utanzu wa mawasiliano
-
Yaani kama ni:
- Hotuba
- Majadiliano
- Masimulizi
- Mazungumzo ya kawaida
- Maelezo
-
Vitathiri mtindo wa uzungumzaji
Sifa ya mzungumzaji
-
Wakati mwingine mtindo wa lugha huathiriwa na sifa za wazungumzaji
-
Sifa hizo zinaweza kuwa:
- Kiwango cha elimu
- Cheo
- Uwezo wa kipato
- Heshima ya mtu katika jamii n.k
Mwalimu
Unasoma somo hili? Niulize nikuelezee chochote kilichomo.
Ingia ili kumuuliza Mwalimu wa AI wa Sonza kuhusu mada hii.
Ingia ili kuuliza