Sonzaschool
Rudi

Sekondari ya Juu · Kidato cha Tano

Kiswahili 1

Rejesta

takriban dakika 1 kusoma

Mada za sehemu hiiMatumizi Ya LughaMada 5

Rejesta

Ni mtindo wa lugha ambayo hutumika mahali penye shughuli fulani, mf: hotelini, shuleni, hospitali, kanisani nk.

Aina za Rejesta

Kuna aina mbalimbali za rejesta kulingana na mahali au shughuli inapofanyika.

  1. Rejesta za hotelini: Huu ni mtindo utumikao hotelini mf: Naniwali kuku? Chai moja chapati moja

  2. Rejesta za mitaani Ni mazungumzo yatumiwayo na aina fulani ya watu katika magenge, vijiweni na hueleweka na watu au wahusika wenyewe. Mf: mshikaji-rafiki, Demu-msichana, umenoa- umekosa, dili maiti - mpango usiofanikiwa.

  3. Rejesta za hospitalini Ni lugha itumiwayo na manesi, madaktari na wagonjwa hospitali. Lengo lake ni kupunguza muda kuwashughulikia wateja wengi. mf: kutwa mara tatu yaani kunywa kimoja asubuhi, mchana na jioni.

  4. Rejesta kanisani Ni lugha ya mahubiri. Sifa yake kubwa haibadiliki. mf: Mapendo – daima, Bwana yesu asifiwe – Amina. Msikitini, mf: Asalam aleikum – Aleikum asalaam

  5. Rejesta mahakamani Mtindo huu hutumika mahakamani. Mf: Mheshimiwa hakimu, Mtuhumiwa, kesi nk.

Dhima za Rejesta

  1. Hutumika kama kitambulisho kwa wazungumzaji Mtu huweza kutambua shughuli baada ya kusikia lugha itumikayo. Mtindo wa sokoni ni tofauti na mahakamani hivyo hutambulisha wazungumzaji.

  2. Hutumika kurahisisha mawasiliano kwa kupunguza muda wa kuhudumia mf: Hotelini kama wateja wengi, Naniwali samaki?, Chai wapi?

  3. Hukuza lugha Msamiati wa lugha huongezeka kupitia rejesta. mf: dawa mpya – ikimaanisha dawa za kupunguza makali ya ukimwi.

  4. Huficha jambo kwa wasiohusika mf: Daktari amuandikiapo majibu mgonjwa sio rahisi mtu asiye katika kada hiyo kuelewa. Mf: BS – kupima malaria Stool – kupima choo Inj – Sindano 5/7 – kunywa dawa kwa siku 5 katika wiki

  5. Hupamba lugha Mikato ya maneno katika rejesta inapamba lugha. mf: Wali kuku, wapi mkia

  6. Hutumika kupunguza ukali wa maneno mf: Kujifungua – kuzaa

Mwalimu

Unasoma somo hili? Niulize nikuelezee chochote kilichomo.

Ingia ili kumuuliza Mwalimu wa AI wa Sonza kuhusu mada hii.

Ingia ili kuuliza