Mada za sehemu hiiKuwasiliana Katika Miktadha MbalimbaliMada 4
- Kuanzisha na kuendeleza mazungumzo katika miktadha mbalimbali
- Kutumia maandishi katika mawasiliano
- Matumizi Ya Msamiati Katika Maandishi
- Matumizi ya Msamiati Katika Mazungumzo
Majina ya Vinywaji
Vinywaji visivyo na vilevi
Faida
-
Maji
- Hukata kiu
- Husaidia kuyeyusha chakula mwilini
- Ni sehemu ya uhai
-
Maji ya matunda (juisi)
- Hukata kiu
- Hutibu magonjwa
- Huwafaa watoto na wagonjwa
-
Soda
- Hutuliza kiu
- Huongeza sukari mwilini
Hasara
- Vinywaji vyenye sukari nyingi vina madhara mwilini mwetu
- Huongeza sukari isiyotakiwa mwilini
Tahadhari
Vinywaji vyenye sukari nyingi yatupasa kuvinywa kwa tahadhari
Vinywaji vyenye kilevi (Pombe)
(a) Pombe za kienyeji
- Wanzuki
- Mbege
- Dengelua
- Mnazi
- Ulanzi
Faida
- Huwa na lishe kidogo
- Hutengenezwa na nafaka (baadhi)
- Hutuliza kiu
- Huwaburudisha wanywaji
Hasara
- Nyingi huwa chafu zikiandaliwa vibaya
- Husababisha magonjwa kama kuhara
- Hupoteza pesa kwa walevi
- Kudhoofisha afya ya mnywaji
- Mlevi huweza kupungua uzito akinywa sana gongo
(b) Pombe za viwandani
- Bia
- Wiski
- Konyagi
- Kilimanjaro
Faida
- Hutuliza kiu
- Hutumika kuburudisha wanywaji
- Hutumika kuwaweka watu pamoja
Hasara
- Hutumia pesa nyingi
- Hudhoofisha afya
- Huchangia kuongeza uzembe
- Walevi wanaweza kupata kisukari
Mimea katika Mazingira Yetu
- Miti ya matunda
- Miti ya mapambo na kivuli
- Mimea ya maua
- Mimea ya mbogamboga
Mti wa kivuli na mimea ya maua
Faida za mimea
- Hutupatia kivuli
- Hutupatia hewa safi
- Hutupatia dawa
- Hutupatia Chakula
Nyakati
Nyakati zimegawanyika katika sehemu kuu tatu ambazo ni:-
- Wakati uliopita
- Wakati uliopo
- Wakati ujao
| Wakati | Silabi ya wakati | Tendo |
|---|---|---|
| Uliopita | -li- | Tulikula, Alikula |
| Uliopo | -na- | Tunakula, Wanakula |
| Ujao | -ta- | Tutakula, Watakula |
Kutunga sentensi za wakati uliopita
Tutatumia —li-
- Juma alifundishwa kusoma
- Mama alipika pilau tamu sana
- Juzi tulikula wali na kisamvu
- Asubuhi niliamshwa mapema
- Babu alifurahi alipotafuna bisi
- Dada alinunua nyanya gengeni
Mwalimu
Unasoma somo hili? Niulize nikuelezee chochote kilichomo.
Ingia ili kumuuliza Mwalimu wa AI wa Sonza kuhusu mada hii.
Ingia ili kuuliza