Mada za sehemu hiiKuwasiliana Katika Miktadha MbalimbaliMada 4
- Kuanzisha na kuendeleza mazungumzo katika miktadha mbalimbali
- Kutumia maandishi katika mawasiliano
- Matumizi Ya Msamiati Katika Maandishi
- Matumizi ya Msamiati Katika Mazungumzo
Hadithi ya ndege
Hapo kale ndege waliishi porini, ndege hao walioishi porini ni tausi, tai, flamingo, kangaroo, kanga, chiriku, mbuni na kasuku. Wote hao walikuwa wanaishi porini. Kuku, bata, njiwa na kware makazi yao yalikuwa kwenye vichaka, miti, nyasi na porini.
Siku zilipita maisha yakaanza kuwa magumu sana. Wadudu walianza kupungua, mazao shambani yakakauka, majani yakakauka kutokana na ukame. Ndege wengi walikufa waliobaki walidhoofu.
Siku moja kuku aliwakusanya ndege wote, akasema ndugu zangu ninashukuru kwa kuja. Lengo la wito ni kuwaasa kuwa kutokana na hali ilivyo inatubidi tukajisalimishe kwa binadamu. Huenda akatupa hifadhi, chakula na kuweza kutunusuru maisha yetu na watoto wetu.
Mbuni alidakia hoja we kuku vipi? Unataka twende kwa binadamu akatufanye kitoweo? Hapana siendi, bundi nave akadakia hata mimi siendi kunguru akacheka kwa! Kwa! Kwa! Yaani bundi huendi unaogopa nini wakati mimi na wewe hatumpati binadamu?
Bata, Kware na Njiwa wao wakasema wataenda hivyo hivyo kama kufa na tufe tu. Mabishano yaliendelea na mwisho kuku akatumwa aende akatafute kwanza kisha arudi kuwapa wenzake jibu. Kuku hakurudi, basi kanga akasema na mimi namfuata nitajua kama ametusaliti ama kunajanga limempata. Hivyo basi kanga alienda anamuita kuku wee! Kuku wee! Kuku wee! Mpaka leo. Ikafika zamu ya mwewe kumfuata akakuta watoto wa kuku wamenenepa mno! Loo! L'roho ukamshika akaanza kuwawinda mpaka leo.
Bundi akasema, nitakwenda usiku, nitakaa kwenye paa ya nyumba ya binadamu nimtishe akimbie mpaka leo bundi hajafanikiwa
Majina mengine ya ndege ni:
- Bata
- Bata mzinga
- Chiriku
- Bundi
- Kware
- Kuku
- Kunguru
- Mbuni
- Kasuku
- Tai
- Tausi
- Korongo
- Flamingo
Kuandika kifungu cha habari na kubaini maneno haya
Vijana wengi wa siku hizi wana mambo mengi wanayopitia. Eti wanasema wanakwenda na wakati na utandawazi pia wengine wanaeleza kuwa wanaendana na maendeleo ya mtandao. Kila mtu ana wazo lake, wengine usiku na mchana ni kutuma ujumbe kupitia simu zao, na wengine kupiga picha hadi moto wote unaisha.
Ukiwaona wanavyovaa, hapo utacheka wanaume wanavaa mlegezo mpaka unaogopa unadhani kuwa suruali inataka kuanguka lakini wapi! Wengine wanavaa nguo kama utumbo zimetepeta na kulegea kama mfuko au utadhani wamejisaidia haja kubwa humo.
Mbaya zaidi wengine wamesuka nywele kama wadada, wametoboa pua na kufunga vipuri na walionyoa basi wamenyoa ovyo ovyo.
Kuorodhesha maneno mapya
- Utandawazi
- Mtandao
- Mlegezo
- Kutepeta
- Vipuri
- Shuleni
- Hospitali
Katika kijiji chetu cha kisiwani mvua kubwa ikinyesha huwa shughuli zote za kibinadamu husimama kwani hali huwa mbaya sana na kusababisha maji kujaa baadhi ya sehemu.
Tuna shule mbili za msingi Baraka na Maua huwa zinafungwa wakati wa masika. Masomo husimama mpaka mvua ziishe na mafuriko kuisha. Hali hii huwa inaumiza sana kwa sababu huwa tunakosa masomo na kupoteza muda mwingi nyumbani.
Pia zahanati yetu huwa inajaa maji kiasi kwamba watu wanashindwa kutoka na kuingia hali hii huwa mbaya kwa wagonjwa wanaohitaji matibabu wakati huo.
Kiwanja cha mpira cha shule ya msingi Baraka kimekuwa kama bwawa la kufugia samaki. Michezo na mazoezi yamesimama afya za watu hazipo salama. Tunapenda michezo lakini viwanja havipo mahali salama.
Wakati huo mashamba ya mpunga na bustani za mboga vyote vimekumbwa na mafuriko, mpunga umelazwa matopeni, mboga zote zimeharibika na maji, hakuna kinachofaa. Tutakufa kwa njaa mwaka huu, mvua imeharibu mashamba yote hapa Kisiwani.
Mwalimu
Unasoma somo hili? Niulize nikuelezee chochote kilichomo.
Ingia ili kumuuliza Mwalimu wa AI wa Sonza kuhusu mada hii.
Ingia ili kuuliza