Mada za sehemu hiiMaendeleo Ya KiswahiliMada 3
- Nadharia kuhusu chimbuko la kiswahili
- ushahidi wa kihistoria
- Ukuaji na ueneaji wa kiswahili duniani
Neno asili lina maana kuwa jinsi kitu au jambo lilivyotokea au lilivyoanza na tunapozungumzia asili ya lugha ya Kiswahili ina maanisha tunachunguza namna lugha hiyo ilivyoanza. Wataalamu mbalimbali wa lugha wamefanya uchunguzi juu ya asili ya lugha ya Kiswahili. Uchunguzi huo umejenga nadharia mbalimbali zinazoelezea chimbuko la lugha ya Kiswahili. Kwa ujumla historia kuhusu asili ya lugha ya Kiswahili ina matatizo mengi na ndiyo maana kuna nadharia mbalimbali zinazoelezea juu ya asili ya lugha ya Kiswahili.
Miongoni mwa matatizo yanayoikabili historia ya Kiswahili ni pamoja na:
- Hakuna uthibitisho kamili juu ya nadharia zinaelezea asili ya lugha ya Kiswahili na kuenea kwake.
- Uchunguzi wa asili ya Kiswahili ulifanywa na wataalamu wa kizungu ambao waliandika historia ya Kiswahili jinsi walivyoelewa wao baada ya kupata ushahidi kidogo tu.
- Wazawa hawakushirikishwa ipasavyo katika uchunguzi wa lugha ya Kiswahili.
- Hapakuwa na kumbukumbu za kutosha kwa sababu babu zetu hawakujua kusoma wala kuandika hivyo basi kuna upungufu wa kumbukumbu.
Kutokana na matatizo hayo yanayoikabili historia ya Kiswahili kuna nadharia mbalimbali zinazoelezea historia ya lugha ya Kiswahili. Nadharia hizo ni kama vile:-
- Kiswahili asili yake Kongo
- Kiswahili ni kundi au pijini
- Kiswahili ni lugha ya vizalia
- Kiswahili ni Kiarabu
- Kiswahili ni Kibantu
Baadhi ya wataalamu hudai kuwa asili yake ni Kongo (Zaire). Madai haya yanaimarishwa zaidi na wazo jingine linalodai kwamba katika vipindi lengwa vilivyopata kuwepo sehemu za Pwani ya Afrika Mashariki hazikuwa zimekaliwa na watu. Lakini kutokana na hali ya uzito, ufugaji, na biashara inadaiwa kuwa wabantu walisambaa Afrika Mashariki kupitia Kigoma na baadhi ya sehemu za Uganda. Wakati wa kusambaa kwao walieneza pia lugha zao kikiwemo Kiswahili.
UDHAIFU
Madai kuwa asilia ya Kiswahili ni Kongo hayana msingi kwa sababu mpaka sasa wataalamu wa nadharia hiyo hawajaweza kueleza na kuthibitisha kisayansi ama kihistoria juu ya lini hasa watu walianza kuishi Pwani ya Afrika Mashariki.
Baadhi ya wataalamu hudai kuwa asilia ya Kiswahili ni tokeo la mwingilio baina ya wenyeji wa Pwani ya Afrika Mashariki na wageni wa kiarabu. Wataalamu hawa hudai kuwa Kiswahili ni lugha ya kati iliyozuka ili kurahisisha au kufanikisha mawasiliano katika shughuli ya biashara ya mwanzo. Wataalamu hawa husisitiza kuwa lugha ya Kiswahili haikuwepo kabisa kabla ya hapo. Wanaona lugha ya Kiswahili ilianza kama pijini na baadaye kukua na kuwa kama Krioli kutokana na lugha hiyo kuwa lugha ya mwanzo kwa wazungumzaji.
Pijini ni nini?
Ni lugha ambayo huzuka kutokana na kuwepo pamoja kwa makundi mawili yanayotumia lugha mbili tofauti. Ili makundi hayo yaweze kuwasiliana, huundwa lugha ambayo kitabia ni tofauti na zile zinazozungumzwa na makundi yanayohusika. Lugha hii inaweza kuwa na msamiati kutoka katika lugha moja kati ya hizo mbili, au inaweza ikawa na msamiati wenye uzito sawa. Lugha hii ndiyo huitwa Pijini. Pijini huzuka kutokana na vitu kama vile biashara, utumwa, ukoloni, n.k
Krioli ni nini?
Kwa kawaida watu wanaozungumza lugha ya pijini wanaweza kuzoeana na kuishi kwa pamoja hata kuoana. Watoto watakaozaliwa hutumia lugha ya pijini kama lugha yao ya kwanza. Lugha hii inayotumiwa na watoto hawa watakaozaliwa huitwa krioli. Krioli ni pijini iliyokomaa.
Wataalamu wa nadharia hii hutumia kigezo cha msamiati uliopo katika lugha ya Kiswahili ambao kwa kiasi kikubwa unatoka katika lugha ya Kiarabu. Ni kweli kuwa lugha hii inamchango mkubwa wa msamiati katika lugha ya Kiswahili.
UDHAIFU
Hutumia kigezo kimoja cha msamiati peke yake kama kigezo pekee ni udhaifu kwa kuwa lugha inaweza kutazamana kwa kutumia vigezo vingine, matamshi, maumbo ya maneno au miundo ya sentensi. Ukitumia vigezo mbalimbali vya uchambuzi wa lugha, lugha ya Kiswahili ina mfanano zaidi na lugha za kibantu kuliko madai yaliyotolewa na nadharia hii.
Kuna madai kwamba lugha ya Kiswahili asilia yake ni Kiarabu. Wataalamu wa nadharia hii hutetea madai yao kwa hoja kuu tatu:-
- Idadi kubwa ya maneno yaliyomo katika Kiswahili takribani 30% ni maneno yenye asilia ya Kiarabu. Hivyo basi ni uthibitisho tosha kwamba Kiswahili kilianza kama pijini ya Kiarabu.
- Neno lenyewe, Kiswahili; ambalo asilia yake ni Kiarabu. Neno Kiswahili limetokana na neno 'sahil' ambalo ni neno la Kiarabu lenye maana ya 'Pwani' na neon 'Swahili' hutumika likiwa na maana ya 'Pwani". Kwa hiyo neno, 'waswahili' lina maana 'watu wa pwani'.
- Dini / Biashara / Mila na desturi. Inadaiwa kwamba kwa kuwa Kiswahili kilianzia Pwani na kwa kuwa kuna idadi kubwa ya wenyeji wa Pwani ni waislamu kwa imani zao, na kwa kuwa uislamu uliletwa na waarabu, basi hata Kiswahili nacho kililetwa na waarabu.
UDHAIFU
- Kutumia kigezo cha msamiati ni udhaifu kwa sababu kila lugha huchukua msamiati kutoka lugha nyingine. Kiswahili hakikuchukua msamiati kutoka Kiarabu pekee kutoka lugha nyingine kama: Kiajemi, Kireno, Kihindi, Kijerumani na Kiingereza.
- Lugha huchukua msamiati mwingi kutoka lugha fulani si kigezo cha kuhalalisha kuwa lugha fulani ina asilia fulani mfano: Kiingereza huchukua maneno kutoka lugha ya Kifaransa, haiwezekani kuhitimisha kuwa Kiingereza ni Kifaransa.
- Pia kutumia kigezo cha dini ni udhaifu. Kwa mfano hatuwezi kusema Kiingereza ni Ukristo kwa kuwa Waingereza ni Wakristo kwa imani yao. Pia nchi kama Senegal ambayo ina Waislamu wengi lugha ya Kiswahili haizungumzwi huko. Ni wazi kuwa Uislamu ungekuwa unafungamana na Kiswahili, kingezungumzwa kila sehemu ambapo Uislamu umeenea.
Nadharia hii hutumia ushahidi wa kiisimu na kihistoria kuchunguza lugha ya Kiswahili katika mfumo mzima wa kihistoria wa mgawanyiko na usambaaji wa lugha za kibantu. Nadharia hii inaungwa mkono na wataalamu kama Malcom Guthrie, C. Meinhoff na C. Rohl. Wataalamu hawa huhitimisha kuwa Kiswahili ni mojawapo ya lugha ya jamii kubwa ya lugha za kibantu. Nadharia hii ndiyo inaelekea kukubalika- kwa wengi kuwa ndiyo sahihi katika kuelewa asilia ya Kiswahili. Kwa sababu nadharia hii imethibitishwa kwa hoja za kiisimu na hoja za kihistoria.
USHAHIDI WA KIISIMU
Ushahidi wa kiisimu ni ushahidi unaothibitishwa kwa misingi ya sayansi ya lugha. Isimu huchunguza lugha kwa undani kwa kutumia tanzu zake. Baada ya kufanyiwa utafiti wa kina na wataalamu mbalimbali, ilithibitika kuwa asilia ya Kiswahili ni kibantu kutokana na vingezo vifuatavyo:-
-
Utafiti wa Malcom Guthrie ni mtaalamu wa isimu kutoka chuo kikuu cha London, aliyefanya utafiti wa kutafuta uhusiano kati ya lugha ya Kiswahili na lugha za kibantu kwa miaka 20 katika nchi za Kiafrika zilizopo Kusini mwa Jangwa la Sahara ambazo zinasadikika kuwa ndipo wabantu wanapoishi.
-
Katika utafiti wake alichunguza mizizi ya maneno 22,000 kutoka lugha za Kibantu ikiwemo lugha ya Kiswahili
-
Katika utafiti wake aligundua mambo yafuatayo:-
- Mizizi 2,300 ilizagaa katika lugha mbalimbali za kibantu ikiwemo lugha ya Kiswahili.
- Mizizi 500 iliungana katika lugha zote 200 alizozifanyia utafiti.
- Alipolinganisha lugha hizo na lugha ya Kiswahili, zilionesha ulinganifu kama ifuatavyo:-
| Lugha ya Kibantu | Kilinganisho na Kiswahili (%) |
|---|---|
| Kiwemba (Zambia) | 54 |
| Kiluba (Katanga) | 51 |
| Kikongo (DRC) | 44 |
| Kiswahili cha Afrika Mashariki | 44 |
| Kisukuma (Tanzania) | 41 |
| Kiyao (Tanzania, Msumbiji) | 35 |
| Kirundi (Burundi) | 43 |
| Kisotha (Botswana) | 20 |
Mtaalamu huyu pia aligundua kadri unavyoshuka Kaskazini ya Katanga ndiyo msamiati unavyoachana zaidi,
Mfanano wa msamiati
Ushahidi huu ulitokana na utafiti wa Prof. Maganga ambaye alibaini kuwa 60% ya maneno ya Kiswahili yenye kuandikika na kutamkika, yana asilia ya Kibantu. 30% ya msamiati wa lugha ya Kiswahili unatoka katika Kiarabu na 10% inatoka katika lugha nyingine mfano: Kireno, Kiingereza.
Ni wazi kuwa msamiati wa Kiswahili na Kibantu hautofautiani sana, hasa katika matamshi.
Miundo ya tungo
Miundo ya tungo za maneno ya Kiswahili inafanana na miundo ya tungo za maneno ya Kibantu. Mfano: miundo ya sentensi za Kiswahili huwa na muundo wa Kiima na kuarifu hali kadhalika miundo ya sentensi za Kibantu huwa na muundo huo huo.
Mfano:-
| Kiswahili | Kisukuma | Kinyakyusa | Kihehe | Kiha |
|---|---|---|---|---|
| Mama anakunywa maji | Mayo aling'hwa minze | Jubha ikonwa amesi | Yubha inywa lulenga | Mawe ang'wa mazi |
NB: Pia miundo ya sentensi za Kiswahili hubadilika katika maumbo ya umoja na wingi. Pia maumbo ya kibantu hubadilika katika maumbo ya umoja na wingi.
Mfano: Watoto wanakunywa maji (Kiswahili)
| Kiswahili | Kinyakyusa | Kihehe | Kisukuma (umoja) | Kisukuma (wingi) |
|---|---|---|---|---|
| Mwana mnunu ikonwa amesi | Mwana ikonwa amesi | Mwana avana vinywa lulenga | Ng'wana aling'wa minze | Bhana bhaling'wa minze |
Ngeli za majina
Makundi ya majina mbalimbali katika lugha ya Kiswahili huwa na makubaliano kwa kufuata maumbo ya umoja na wingi pamoja na upatanisho wa kisarufi. Tabia hizi za majina ya Kiswahili hujitokeza pia katika majina ya Kibantu;
Kwa kutumia maumbo ya majina. Majina mengi ya Kiswahili huwa na maumbo ya umoja na wingi, halikadhalika kwa majina mengi ya Kibantu.
Mfano:
| Kiswahili | Kisukuma | Kinyakyusa | Kihehe |
|---|---|---|---|
| m-toto wa-toto | ng'-ana bh-ana | mw-ana b-ana | mw-ana v-ana |
| ki-ti vi-ti | ki-goda vi-goda | ki-goda vi-goda | ki-kota vi-kota |
Kigezo cha upatanisho wa kisarufi
Kwa kutumia kigezo hiki, nomino za Kiswahili na za kibantu hufuata upatanisho wa kisarufi kwa kupachika viambishi pia. Viambishi hivyo hubadilika kutokana na mabadiliko ya maumbo ya umoja na wingi.
Mfano:
- Mtoto mzuri anakunywa maji
- Watoto wazuri wanakunywa maji
- Mwana mnunu ikonwa amesi
- Bana banunu bikonwa amesi
- Mwana mnofu inywa lulenga (umoja)
- Vana vanofu vinywa lulenga (wingi)
Vitenzi vya Kiswahili na vya Kibantu
Tabia ya vitenzi hivi hufanana. Mfanano huo hujitokeza katika vipengele vifuatavyo:-
-
Viambishi Lugha ya Kiswahili na kibantu, vitenzi vyake huwa na mzizi pamoja na viambishi awali na tamati.
Mfano:
Kiswahili Kindali Kikurya a-na-lim-a a-ku-lim-a a-ra-rem-a 1 - viambishi vya nafsi 2 - Viambishi vya wakati 3 - mzizi 4 - Viambishi tamati maana.
-
Vitenzi vya lugha ya Kiswahili na Kibantu vina tabia ya kunyumbuka
Kiswahili Kinyamwezi Kindali Kipogoro Kibena Kucheka Kuseka Kuseka Kuseka Kuheka Kuchekesha Kusekesha Kusekesha Kusekesa Kuhekesha Kuchekelea Kusekelela Kusekelela Kusekelela Kuhekelela Kuchekwa Kusekwa Kusekwa Kusekwa Kuhekwa -
Mwanzo wa vitenzi Vitenzi vya Kiswahili na Kibantu huanza na viambishi vya nafsi mwanzoni.
Mfano: Ni nakwenda
- ni - sumwike
- ni - ngenda
-
Mwisho wa vitenzi Vitenzi vingi vya lugha ya Kiswahili na vile vya kibantu, huishia na irabu ('a') mwishoni.
Mfano:
Kiswahili Kisukuma Kihehe Kukimbia Kupila Kukimbila Kuwinda Kuhwima Kufwina Kushuka Kutenda Kuwika
Mwalimu
Unasoma somo hili? Niulize nikuelezee chochote kilichomo.
Ingia ili kumuuliza Mwalimu wa AI wa Sonza kuhusu mada hii.
Ingia ili kuuliza