Mada za sehemu hiiTungoMada 2
- Sentensi
- Kuchanganua Sentensi
Sentensi ni kifungu cha maneno kuanzia neno moja na kuendelea, chenye kiima na kiarifu, na kinaleta maana kamili. Sentensi ndiyo kipashio cha juu kabisa katika daraja la vipashio vya lugha. Muundo wa sentensi una sehemu kuu mbili:
- Kiima
- Kiarifu (kikazi/kidhima)
Muundo wa sentensi (Kimuundo):
- Kiima (KN)
- Kiarifu (KT)
Kiima ni sehemu au nafasi inayokaliwa na nomino au kikundi nomino ambacho kinaweza kujulikana mara nyingi kuwa mtenda.
Mfano:
- Ali amewapiga watoto.
- Yeye ananitukana.
- Mkulima na bwana shamba wamelima kwa pamoja.
Vipashio vya Kiima
Kiima huundwa na:
- Jina (N): Mfano: Mtoto anacheza mpira.
- Jina na jina (N + N): Mfano: Baba na mama wanalimia.
- Jina + kishazi tegemezi kivumishi (N + V): Mfano: Kitu kinachompendeza ni kuwa na nguo nzuri.
- Kivumishi na jina (V + N): Mfano: Yule mtoto ni mzuri.
- Kiwakilishi peke yake: Mfano: Wewe huna matatizo.
- Kitenzi jina: Mfano:
- Kilimo cha kufa na kupona kinaanzishwa nchini.
- Kuimba na kucheza kwako kunafurahisha.
- Kuiba hakupendezi.
- Jina + kivumishi: Mfano: Watoto wote ni watundu.
Kiarifu ni sehemu inayokaliwa na maneno yanayoarifu funzo lililofanywa, linalofanywa, au litakalofanywa. Kiarifu pia ni sehemu inayokaliwa na kishirikishi peke yake au kitenzi kikuu kimetumika sambamba na kitenzi kisaidizi kimoja au zaidi.
Mfano: Kaka alikuwa anaumwa.
Vipashio vya Kiarifu
- Kitenzi kikuu: Mfano:
- Haji atalima kesho asubuhi.
- Karama anacheza mpira.
- Kitenzi au vitenzi visaidizi vinavyoambatana na kitenzi kikuu: Mfano:
- Mtoto alikuwa analima kila mara.
- Wavulana walikuwa wamekwisha kula.
- Kitenzi kishirikishi na nomino: Mfano:
- Juma ni mtoto.
- Mtoto ni mgonjwa.
Shamirisho ni sehemu au nafasi inayokaliwa na nomino au kikundi nomino ambacho kinaweza kujulikana kuwa ni mtendwa, mtendewa, au kitendwa (a/a).
Mfano:
- Juma amempiga mtoto (Mtendwa).
- Mwalimu amempa mtoto zawadi (Mtendewa).
- Mwalimu amempiga mtoto fimbo (Mtendwa).
Chagizo ni sehemu au nafasi inayokaliwa na kiulizi au kikundi kielezi. Chagizo huweza kutokea baada ya kitenzi kikuu au shamirisho.
Mfano:
- Juma ataondoka kesho.
- Mama anasoma kitabu polepole.
Sentensi Sahili
Hii ni sentensi ya kishazi huru, kishazi hiki kinaweza kuwa na kifungu kitenzi kimoja, kifungu kitenzi hicho kinaweza kuwa cha kitenzi kikuu, kisaidizi, au kishirikishi.
Mfano:
Sentensi Changamano
Hii ni sentensi inayoundwa na kishazi huru kimoja au zaidi na kishazi tegemezi kimoja au zaidi.
Mfano: Nyumbu aliyepigwa risasi amekufa.
Miundo ya Sentensi Changamano:
- Muundo wenye Kishazi Tegemezi Vumishi: Mtoto anayeumwa kichwa amepona. Kisu kilichopotea juzi kimepatikana leo asubuhi.
- Muundo wenye Kishazi Tegemezi Kielezi: Juma alikimbia aliponiona. Saidi hataki kununua matunda sokoni.
Sentensi Ambatano
Hii ni sentensi ambayo huundwa na sentensi mbili au zaidi ambazo huunganishwa kwa kiunganishi.
Miundo ya Sentensi Ambatano:
- Muundo wa Sentensi Sahili (Vishazi Huru) Viwili au Zaidi Vilivyoambatanishwa kwa Kutumia Viunganishi:
- Mama analima na baba anapanda.
- Yeye anapenda kusoma na mwanawe anapenda kucheza.
- Juma ni mrefu lakini Saidi ni mfupi.
- Sentensi Sahili (Kishazi Huru) Pamoja na Tungo Changamano:
- Mtoto aliyekuja jana amekwenda sokoni lakini mama yake anapika jikoni.
- Msichana uliyemwona juzi ameondoka na mimi nimefurahi ameondoka salama.
- Muundo Wenye Sentensi Changamano Mbili Zilizounganishwa kwa Kiunganishi:
- Ng'ombe aliyezaa amepotea na ndama aliyezaliwa amekufa.
- Mtoto aliyesimama njiani ni mwanangu lakini yule aliyekaa chini ni mwanafunzi.
- Miundo Yenye Vishazi Visivyo Uunganishwa kwa Viunganishi:
- Niambie, niondoke.
- Mwache, aende tu.
- Mfundishe, aelewe.
Sentensi Shurutia
Hii ni sentensi ambayo ina vishazi tegemezi viwili ambavyo hutegemezi wake hutokana na mofimu –nge, –ngali, –ngeli, –ki.
Mfano:
- Angejibu maswali angefaulu mtihani.
- Juma angelikuja mapema angelimkuta Mussa.
Mwalimu
Unasoma somo hili? Niulize nikuelezee chochote kilichomo.
Ingia ili kumuuliza Mwalimu wa AI wa Sonza kuhusu mada hii.
Ingia ili kuuliza