Sonzaschool
Rudi

Sekondari ya Kawaida · Kidato cha Tatu

Kiswahili

Kuchanganua Sentensi

takriban dakika 3 kusoma

Mada za sehemu hiiTungoMada 2
  1. Sentensi
  2. Kuchanganua Sentensi

Uchanganuzi wa Sentensi

Kuchanganua sentensi ni mbinu ya kuigawa sentensi katika sehemu mbalimbali ambazo huunda sentensi hiyo.

  1. Kutaja aina ya sentensi yaani kama ni sentensi sahili, ambatano au changamano.

  2. Taja sehemu zake kuu yaani; kiima na kiarifu (kishazi) au KN na KT (kimuundo)

  3. Kama ni sentensi sahili onyesha vipashio vya kiima na kiarifu; yaani jina, vivumishi, vitenzi, shamirisho na chagizo n.k

    Kama ni sentensi changamano taja vishazi vyake na kazi ya kila kishazi tegemezi katika hiyo sentensi changamano yaani taja: kama kishazi tegemezi kinavyovumisha jina au KN kilicho katika kiima au KN cha kishazi huru. Mfano; Mzee uliyemwona jana ni baba yangu.

    "uliyemwona jana" ni kishazi tegemezi kivumishi kinachovumisha jina "mzee" lililo kiima cha kishazi huru (K/H) "mzee ni baba yangu"

  4. Kutaja aina za maneno yote yaliyomo katika sentensi hiyo.

    Mfano; Baba na mama wanakula ugali

    N t N T N

  5. Kuandika tena sentensi

Mwalimu

Unasoma somo hili? Niulize nikuelezee chochote kilichomo.

Ingia ili kumuuliza Mwalimu wa AI wa Sonza kuhusu mada hii.

Ingia ili kuuliza