Sonzaschool
Rudi

Msingi · Darasa la Tano

Kiswahili

Muundo wa vitendawili

takriban dakika 1 kusoma

Mada za sehemu hiiVitendawiliMada 3

Vitendawili

Vitendawili ni tungo au semi fupifupi zilizofumbwa na hutumia lugha ya picha kuelezea wazo lililofichika. Kitendawili uhusisha watu wawili yaani mtegaji na mteguaji.

Muundo wa vitendawili

  • Kitendawili (mtegaji) — swali au kile anachosema mtegaji
  • Tega (mteguaji) — jibu la kitendawili

Kwa mfano:

  • Popo mbili zavuka mto — Kitendawili (mtegaji)
  • Macho — Tega (mteguaji)

Ikiwa mteguaji amekosa jibu hupaswa kumchagua mji mtegaji na mtegaji akiridhika na mji aliopewa hutoa jibu la kitendawili alichotega.

Vitendawili huundwa kwa taswira na tamathali za semi

  • SITIARI — Nyumba yangu ndogo lakini wapangaji wengi — kiberiti
  • DHIHAKA — Kitu kidogo kimemtoa mfalme kitini — haja
  • TANAKALI — Huku pi na kule pi — mkia wa kondoo anapotembea
  • TASWIRA — Babu yangu kalala kaacha ndevu nje — muhindi
  • TASHIHISi — Popo mbili zavuka mto — macho

Mwalimu

Unasoma somo hili? Niulize nikuelezee chochote kilichomo.

Ingia ili kumuuliza Mwalimu wa AI wa Sonza kuhusu mada hii.

Ingia ili kuuliza