Mada za sehemu hiiUundaji Wa ManenoMada 3
- Mofimu
- Uambishaji
- Mnyambuliko
Unyambulishaji unatokana na neno "nyambua" ikiwa na maana refusha au vuta kitu. Mnyambuliko ni kitendo cha uvutaji au urefushaji kipashio / vipashio katika mzizi wa neno. Aidha mnyambuliko unahusu upachikaji wa mofimu zinazofuata mzizi wa neno. Mofimu hizi huitwa mofimu fuatishi (viambishi tamati)
Mfano:
- Soma - som-e-a
- Som-eka
- Som-esha
- Som-wa
- Som-eana
- Som-o
Vitenzi vyote vya Kiswahili isipokuwa kitenzi kishirikishi "ni" vinaweza kunyambulika.
Mfano:
Piga - pigia, pigana, pigisha, pigwa, pigiana, cheza, chezea, chezeana, chezeshwa, chezwa
Baadhi ya majina ya ujumla hupokea viambishi tamati na mengine hupokea viambishi tamati vijenzi.
Mfano:
- Nyumba - nyumbani
- Bustani - bustanini
- Hewa - hewani
- Maji - majini
Hivi huchukua viambishi tamati maana
Mfano:
Viwakilishi vya nafsi kama vile
- Mimi - miye
- Wewe - weye
- Sisi - siye
- Ninyi - niye
Viwakilishi virejeshi vya amba
- Ambalo
- Ambacho
- Ambavyo
Hivi huchukua viambishi tamati vijenzi
Mfano:
- Safi - safisha, safishwa, safishia, safishika
- Fupi - fupika, fupisha, fupishika, fupishwa
- Refu - refusha, refushwa, refushika
Hesabu ndogo ya viunganishi huchukua viambishi tamati vitenzi.
Mfano:
Labda, labdatisha, labdilika, labdishwa
- Mnyambuliko wa maneno hukuza msamiati wa lugha husika.
- Mnyambuliko wa maneno hupanua maana ya maneno.
- Mnyambuliko wa maneno huzalisha kauli mbalimbali za vitenzi kutenda, kutendwa, kutendea, kutendeka, kutendana, kutendeana kutendesha, kutendeshwa.
Mwalimu
Unasoma somo hili? Niulize nikuelezee chochote kilichomo.
Ingia ili kumuuliza Mwalimu wa AI wa Sonza kuhusu mada hii.
Ingia ili kuuliza