Mada za sehemu hiiUfahamuMada 1
- Ufahamu wa kusikiliza
Ufahamu ni uwezo wa kuelewa jambo fulani na kuweza kulifafanua.
- Ufahamu wa kusoma
- Ufahamu wa kusikiliza
- Ufahamu wa kutafakari
Ni kuzingatia yote yasemwayo na mtu mmoja, mwingine kusikiliza kunahitaji umakini na utulivu ili kuelewa. Watu huweza kupata taarifa kutokana na kusikiliza jambo husika kwa umakini na utulivu.
Mfano: Mtoto akimsikiliza mwalimu kwa umakini huweza kufanya vizuri kwenye masomo. Hiyo kutokana na kumsikiliza mtu unaweza kupata maarifa, taarifa za kufurahisha au kuhuzunisha.
Kichocho ni ugonjwa hatari sana, vilevile kichocho ni hatari katika jamii kiujumla. Pia kichocho kinaathiri wakubwa na watoto hasa wale wenye umri chini ya miaka 5, 6 na 7. Pia ugonjwa wa kichocho hutokana kwa njia mbalimbali ikiwemo kukojoa kwenye maji machafu, maji taka (mifereji).
Kusoma ni uwezo wa kuelewa maneno yaliyoandikwa. Ufahamu wa kusoma umegawanyika katika makundi mawili:
- Kusoma kimya
- Kusoma kwa sauti
Msomaji anaweza kusoma kwa kutumia njia moja kati ya hizo mbili lengo ni kuelewa jambo au ujumbe aliosoma. Katika kusoma mtu anaweza kupata maarifa au ujumbe mbalimbali wa kufundisha au kuhuzunisha na hata msisimuko kutokana na yaliyosomwa.
- Husaidia katika kuokoa muda
- Husaidia katika kupunguza gharama
- Husaidia kutoa taarifa kwa ufupi na kumwezesha mtu kufuata maagizo
- Husaidia sana kukuza kuelewa miongoni mwa wanafunzi
- Huelimisha
Mwalimu
Unasoma somo hili? Niulize nikuelezee chochote kilichomo.
Ingia ili kumuuliza Mwalimu wa AI wa Sonza kuhusu mada hii.
Ingia ili kuuliza