Mada za sehemu hiiKutumia Msamiti Katika Miktadha MbalimbaliMada 2
- Kusoma Na Kuchanganua Mawazo Yaliyowasilishwa Katika Matini Mbalimbali
- Ufahamu na Kusoma Kimya Kimya
Wanywaji wa pombe hawawezi kuelezea utamu wake ulivyo. Wao hunywa tu na kufurahia ulevi wanaoupata japokuwa wapo wanaosema pombe huongeza maji mwilini, lakini hilo mimi silielewi, maji gani yanalewesha?
Wengine hudai kuwa pombe huondoa mawazo na kumfanya mtu kusahau matatizo yake, hili nalo nalichakachua kichwani naona ni uongo kwa vile pombe huzidisha matatizo. Ikiisha mwilini hali liubaki kuwa kama mwanzo.
Hata hivyo, bado ninaamini kuwa pombe inamadhara mengi kuliko faida. Pombe inamaliza pesa, humfanya mtu kuwa mzembe, husababisha ajali, wengi huwa hawajali usafi, hawajali Watoto wao, chakula chao, mavazi na gharama nyingine. Mimi ninaamini kuwa tusipoendekeza pombe tutapiga hatua kubwa katika maendeleo yetu, yajamii na Taifa kwa ujumla.
Habari hii inataja sana kitu gani?
Habari hii inataja sana pombe
Wengine husema kuwa pombe ina faida gani?
Wengine husema hudai kuwa pombe ina faida ya kuongeza maji mwilini na huondoa kabisa mawazo na kumfanya mtu asahau matatizo yake.
Hatahivyo bado ninaamini kuwa pombe inamadhara mengi zaidi kuliko faida
Je, pombe ni nzuri kwa kila mtu?
Hapana, pombe si nzuri kwa kila mtu
Kama ni nzuri mbaya kuandika faida au hasara
- Inamaliza pesa
- Humfanya mtu kuwa mzembe
- Humfanya mtu asijali watoto wake
Kusoma hadithi kwa sauti kwa kuzingatia alama za uandishi
Hawa ni nyani walioko Mwanza. Nyani hao hupenda kula vitu mbalimbali bila hata kujua vitokako. Nyani akiona ndizi yake, akiona embe lake, akiona mua huo ndio wake kabisaaa na kama kapanda yeye wakati hata mbegu hazijui.
Wasukuma hao walipojua tabia hii ya nyani wakaona kuwa watawapata nyani na kuwafanya kitoweo kwa urahisi. Wakabuni mtego. Wakapika uji wakajaza kwenye ndoo, wakatia sukari nyingi, pamoja na dawa ya usingizi wakaenda kutega sehemu wanazoishi nyani.
Mara tu baada ya kuondoka ile minyani ikashuka ikaenda kulamba uji, wakalambaaa! Wakalamba weeee! Mpaka uji ukaisha......nyani wote wakalala fofofo! Pale pale.
Wasukuma bwana wakaja kuwachukua nyani wao, wakawafunga kamba kiunoni na kuwapeleka jela ambako humkamata mmoja mmoja na kumchinja na kumla. Siku hizi nyani wa kisukuma wakiona ndoo imewekwa na binadamu huiburuza na kutupa kwenye mto.
Mwalimu
Unasoma somo hili? Niulize nikuelezee chochote kilichomo.
Ingia ili kumuuliza Mwalimu wa AI wa Sonza kuhusu mada hii.
Ingia ili kuuliza