Mada za sehemu hiiLugha Na MawasilianoMada 5
- Dhana ya lugha
- Dhana ya lugha ya kiswahili
- Matamshi na lafudhi ya kiswahili
- Ufafanuzi wa aina za maneno
- Maana ya Lugha
NOMINO
-
Nomino ni maneno yanayotaja majina ya watu, wanyama, mahali, vitu n.k.
-
Tabia zake kimuundo:
- Huchukua viambishi.
- Huonyesha ngeli na idadi.
- Hutawala kirai nomino.
-
Mifano: jua, Seif, Morogoro.
Aina za Nomino
- Nomino za pekee – Huchukua herufi kubwa. Mfano: Nyerere, Ali, Singida, Nile.
- Nomino za kawaida – Zinataja vitu vyenye tabia za kifaradhi. Mfano: mtoto, mtu, nyumba.
- Nomino za jumla – Zinataja kundi la vitu. Mfano: jeshi, jamii, kundi.
- Nomino dhahania – Zinataja vitu visivyoonekana. Mfano: njaa, furaha, upepo.
VIWAKILISHI
- Huchukua nafasi ya nomino.
- Hubeba tabia za kinomino: kutawala kirai na kuchukua viambishi ngeli.
- Mifano: wewe, sisi.
Aina za Viwakilishi
-
Viwakilishi nafsi
-
Nafsi huru
- Umoja: Mimi (I), Wewe (II), Yeye (III)
- Wingi: Sisi (I), Ninyi (II), Wao (III)
-
Nafsi viambata (huchangamana na vitenzi)
- Mfano: Ninakuja, Tunakuja, Unakuja
-
-
Viwakilishi vya kumiliki – angu, ako, enu, ake
-
Viwakilishi vya kuuliza – kipi, gani, epi
-
Viwakilishi vya kuonesha – huyu, hawa, kile
-
Viwakilishi vya msisitizo – ndiye, ndiwe, ambaye
VIVUMISHI
- Huambatana na nomino/viwakilishi kutoa taarifa zake.
- Huchukua viambishi ngeli.
- Hutawala kirai vumishi.
Aina za Vivumishi
- Vivumishi vya sifa – zuri, hodari, mkubwa
- Vivumishi vya kuuliza – yupi?, gani?
- Vivumishi vya kumiliki – changu, yetu, yako
- Vivumishi vya kuonesha – hii, wale
- Vivumishi vya idadi – wawili, wengi, kidogo
- Vivumishi vya jina kwa jina – Mwalimu Zakia, Baba Juma
- Vivumishi vya -a- unganifu – nyumba ya baba
- Vivumishi vya -enye-, -enyewe- – mtoto mwenye, nyumba yenyewe
- Vivumishi vya o-te- – nyumba yoyote
- Vivumishi vya –ingine/-engine – kiti kingine, watu wengine
VITENZI
- Hueleza tendo au hali ya nomino.
- Huunda kirai tenzi, huonyesha vipatanisho vya kisanifu.
Aina za Vitenzi
-
Vitenzi vikuu – vinaweza kusimama peke yao. Mfano: anacheza.
-
Vitenzi visaidizi – husaidia kitenzi kikuu. Mfano: alikuwa anacheza.
-
Vitenzi vishirikishi – vinaonesha uhusiano wa maneno. Mfano:
- Juma ni mchezaji
- Mtoto yumo ndani
Aina za Vitenzi Vishirikishi
- Vitenzi vya KUWA – alikuwa, hakuwa, ni, si
- Vitenzi vya kuwa NA – ana, alikuwa na
- Vitenzi vya PO, MO, KO – yupo, yumo, yuko
- Vitenzi vya msisitizo NDI – ndiye, siye
- Vitenzi vya msisitizo AMBA – ambaye, ambao
VIELEZI
- Vielezi hufafanua vitenzi, vivumishi auielezi vingine.
Aina za Vielezi
Vielezi vya namna – polepole, kinyumenyume
- Vielezi vya mahali – magengeni
- Vielezi vya idadi – mara kwa mara
- Vielezi vya wakati – juzi
- Vielezi vingine – vya kasoro, sababu, hali ya masharti
VIUNGANISHI
- Maneno yanayounganisha maneno, virai, vishazi, au sentensi.
- Mifano: na, bali, lakini, pamoja na, ama
VIHISISHI
- Hueleza hisia au vionjo vya moyo.
- Huambatana na alama ya mshangao.
- Mifano: Ah!, Oya!, Oh!, Masalale!, Alaa!
Mwalimu
Unasoma somo hili? Niulize nikuelezee chochote kilichomo.
Ingia ili kumuuliza Mwalimu wa AI wa Sonza kuhusu mada hii.
Ingia ili kuuliza