Mada za sehemu hiiUtungajiMada 4
Utungaji ni pato la akili ya mtu binafsi ambayo hurejeshwa kwa fani kama vile macho, ushairi, tamthiliya au hadithi. Utungaji ni kitendo cha kuyatoa mawazo ubongoni, kuyakusanya na kisha kuyadhihirisha kwa kuyaandika au kuyazungumza. Ni kitendo cha kuunda hoja na kuyapanga katika mtiririko unaofaa katika lugha kwa lengo la kufikisha ujumbe kwa jamii husika.
- Mtunzi analazimika kuelewa kikamilifu mada inayoshughulikiwa.
- Mtungaji lazima azingatie kanuni na taratibu za uandishi.
- Mtungaji anatakiwa kuzingatia mpango mzuri na wenye mantiki wa mawazo kutoka mwanzoni hadi mwishoni.
- Mtungaji anapaswa kuwa na msamiati wa kutosha ili kumwezesha kutumia lugha bora, sanifu, na fasaha.
- Mtunzi anapaswa kuzingatia sarufi ya lugha anayoitumia.
- Mtunzi anapaswa kujali nyakati zinazofaa.
- Mtunzi anapaswa kuwa na uwezo wa kutosha wa kuhusisha yanayoelezwa na hali halisi ilivyo katika jamii kwa mifano dhahiri.
- Utungaji wa mazungumzo
- Utungaji wa maandishi
Utungaji wa mazungumzo unahusisha kujieleza kwa njia ya mdomo kwa lengo la kueleweka.
LENGO
- Hutuwezesha kujieleza kwa ufasaha katika kila fani.
- Hutuwezesha kutumia lugha inayotakiwa katika jamii.
- Hujeba moyo/hali ya kujiamini katika kuzungumza
- Kukuza kiwango cha wasikilizaji kwa makini kutoa uamuzi unaofaa.
- Kutuwezesha kutambua lugha inayofaa katika kujieleza kutokana na lafudhi, shada, matamshi na miundo.
MAMBO YA KUZINGATIA KATIKA UTUNGAJI WA MAZUNGUMZO
- Kusikiliza kwa makini, kuchambua na kuelewa vema mada inayozungumzwa. Kuzungumza kwa umakini na kufafanua kwa umakini mada unayozungumza, anapaswa kuzingatia mpango mzuri wa mawazo wenye mantiki kutoka mwanzo mpaka mwisho.
- Mtunzi anapaswa azingatie hadhira anayozungumza nayo.
- Mzungumzaji lazima awe na uwezo wa kufafanua na kuhusisha anayozungumza na hali halisi ilivyo katika jamii yetu.
- Mzungumzaji anapaswa awe na msamiati wa kutosha utakaomwezesha kutumia lugha bora, kujieleza vizuri na kutunza lugha sanifu na fasaha.
- Ni vizuri mzungumzaji akazingatia sarufi ya lugha anayotumia na kujali nyakati.
Ni uwezo wa kujieleza katika maandishi au uwezo wa kutoa mawazo binafsi na kuyaweka katika kiwakilishi cha maandishi. Utungaji wa kuandika tofauti kidogo na utungaji wa kuzungumza. Tofauti haze hujitokeza katika kiwakilishi uwasilishaji wake. Mazungumzo ya chanzo na kikomo na uhusiano baina ya mwandishi na msomaji. Kutokana na tofauti haze katika utungaji wa kuandika maandishi zaidi yanahitajika ukilinganisha na utungaji wa kuzungumza.
MAMBO YA KUZINGATIWA KATIKA UTUNGAJI WA KUANDIKA
- Mwandishi aelewe vema mambo anayoandika.
- Mwandishi anatakiwa kuzingatia mpango mzuri wa mawazo wenye mantiki kutoka mwanzo hadi mwisho.
- Mtungaji anapaswa awe na msamiati wa kutosha utakaomuwezesha kutumia lugha iliyobora, sanifu na fasaha.
- Mtungaji anapaswa awe na uwezo wa kubebesha yale anayoyaeleza na hali halisi ilivyo katika jamii yetu. Ni vizuri akatoa mifano dhahiri.
- Kuzingatia matumizi bora ya vituo na alama mbalimbali za uandishi kuwa na utangulizi mzuri wenye kuvutia ya watu na hitimisho zuri.
- Mtungaji anapaswa kuzingatia sarufi ya lugha anayoitumia na kujali nyakati.
Alama ya mkato (,)
Alama hii hutumika kwa kazi zifuatazo:
- Kuweka pumziko fupi katika sentensi. Mfano: tulipofika nyumbani, tulikula Chakula.
- Kutenga maneno yaliyo katika orodha. Mfano: ukifika sokoni nunua matunda, dagaa, mkaa, unga, na sabuni ya kufulia.
- Kuonesha sehemu mbili za sentensi zilizo kinyume. Mfano: Sisi wanadamu hupanga, Mungu hupangua. Ulisema utakuja, hukuja
- Kutumiwa kabla ya alama za mtajo. Mfano: Juma alimwambia Khadija, Nakupenda kama pipi.
- Kuonesha vyeo, viwili au masikani baada ya jina la mtajwa Mfano: Philemon Ndesamburo Mbunge wa Moshi mjini, S.L.P 11646, Ngangamfumuni,
Nukta (.)
Alama hii hutumika kama ifuatavyo:
- Hutumika kukamilisha sentensi na hivyo kuweka pumziko kubwa tunaposema. Mfano: Mtoto wangu nampenda sana.
- Kuonesha ufupisho wa maneno. Mfano: S.L.P – Sanduku la posta n.k – nakadhalika
- Kuonesha vipimo mbalimbali katika desimali
Mfano: kg. 80. 3
- Saa 2.30
Nukta mkato (;)
Alama hii hutumika kama ifuatavyo:
- Kuunganisha sentensi mbili zinazoweza kusimama zenyewe bila kutumia kiunganishi. Mfano: Hapo zamani watu walijiheshimu sana; Siku hizi hawajiheshimu kabisa
- Hutumika ili kupumzika katika sentensi iliyondefu sana, kuliko unapotumika mkato. Mfano: Alipomtazama alibaini kuwa alikuwa Malaya wa kutupwa; Hivyo aliamua kuachana naye.
Nukta mbili / pacha (:)
Alama hii hutumika kama ifuatavyo:
- Hutumika kutaja Maneno yaliyo katika orodha. Mfano: Niletee vitu hivi: wino, karatasi, kalamu, kiberiti, daftari, wembe, ndimu, chungwa na ndizi.
- Hutumika badala ya alama ya mkato. Mfano: Alipomwonaianza kumshambulia kwa maneno: "Nakujua wewe huna lolote, mlevi kama wewe!"
- Hutumika baada ya kuandika jina la mhusika katika tamthiliya. Mfano: Julia: Kwame hujui kuwa Nungungungu anavusha kahawa na almasi kwenda nje kwa magendo? Mlemeta: Sijui Julia: Hujui kuwa Nungunungu anaakaunti na hoteli Uswizi?
- Kutenganisha dakika na sekunde. Mfano: Saa 8:30:48
- Kuonesha uwiano baina ya namba. Mfano: Juma na Hamisi waligawana machungwa 20 kwa uwiano ufuatao: 3:7. Je, kila mmoja alipata machungwa mangapi?
Alama ya kushangaa (!)
Alama hii kutumika kama ifuatavyo:
- Hutumika kuonesha vionjo vya moyo kama vile furaha, huzuni, chuki. Mfano: Kumbe Juma alikuwa mwizi wa mitumba!
- Hutumika wakati wa kusisitiza, kubeza, kutunza n.k Mfano: Kwenda! Mwone kwanza alivyo! Uso umemshuka!
Alama ya kuuliza (?)
Alama hii hutumika kama ifuatavyo:
- Hutumika kuuliza maswali. Mfano: Mwalimu leo tutafanya mtihani?
Alama ya mabano [()]
Alama hii hutumika kama:
- Hutumika kuonesha maana ya ziada katika sentensi. Mfano: Wale watoto wangu (Robson, Karen, na Maurene) nawapenda sana.
Alama ya kistari (–)
- Alama hii hutumika kuonesha kuwa neno linaendelea katika mstari unao fuata Mfano: wafanya ka- zi wa shu- le wote.
- Hutumiwa kuzungumza maneno au kujenga neno moja na mtindo huu hutumika zaidi katika maneno yenye asili ya kigeni. Mfano: Idd – Al- Haji Dar – Es – Salaam
- Hutumika kuunganisha sentensi mbili, sentensi ya pili ikiwa ni ufafanuzi wa sentensi ya kwanza. Mfano: Tulipofika hifadhi ya manyara, tuliwakuta simba wamelala – simba dume, jike na watoto wanne.
- Hutumika badala ya nukta mbili. Mfano: Nenda kanunue –dagaa, muhogo, maharage, kuni.
Alama ya mtaja ("")
- Hutumika katika kukazia maneno aliyosema au aliyoandika mtu mwingine. Mfano: "Mwalimu Nyerere alisema, 'Enzi za utawala wangu nilifanya mambo mengi mazuri na mengine ya kujenga kwa kuwa nchi yetu ilikuwa bado changa. Lakini cha kushangaza ninyi mmechukua mambo ya kijinga niliyofanya na mnaacha mazuri niliyofanya. Serikali imeshindwa hata kukusanya kodi!"
- Hutumika kubainisha maneno ya kigeni yanayotumika katika lugha fulani. Mfano: Ilituwia vigumu "kujiexpress" mbele za watu. Tumefikishana mahakamani tatizo ni ugomvi wa "kiamba"
- Hutumika kubainisha maneno ya msimu katika lugha fulani. Mfano: "Alipomcheki" aligundua kuwa ni "changudoa"
Rifaa / kibainishi (')
- Kutofautisha "ng" na "ng" katika baadhi ya maneno. Mfano: ngambo – n'gombe ng'ambo Ngangania – ng'ang'ania Ngarisha – ng'arisha
- Kuonesha kuwa herufi fulani imeachwa katika neno. Mfano: Vuta N'kuvute – vuta n'kuvute Watoto wa mama N'tilie
Nukta katishi / nukta dukuduku (...)
- Hutumika kubainisha mdokezo. Mfano: Nakupenda sana lakini…………………
- Hutumika kuonesha kuwa kuna maneno yaliyotangulia katika tungo. Mfano: ……………fika ofisini mara moja.
Matumizi ya herufi kubwa
- Hutumika kila mwanzo wa sentensi Mfano: Mama njoo
- Hutumika baada ya alama ya nukta, kuuliza, kushangaa. Mfano: "Nani huyo?" Aliuliza mama. Wewe ndiyo! Mwanga sana wewe.
- Hutumika kutaja majina ya kipekee Mfano: Winnie, Abel, Ade, Marco, Concepta, Manoza.
- Majina ya dira Mfano: Mashariki, Kaskazini
- Majina ya vyeo Mfano: Sheikh, Rais, Mwenyekiti
- Ufupisho wa vyama, mashirika, jumuiya Mfano: UN, CHADEMA, HKL, ECOWAS
- Majina ya vitabu na mada Mfano: "JE, TUTAFIKA?" "USHUHUDA WA MIFUPA", Mfadhili.
- Majina ya sikukuu Mfano: Krismass, siku ya wapendanao
- Majina ya nafsi yanapotumika kuleta maana maalum.
Aya
Ni jumla ya sentensi zinazoelezea wazo moja na hufanya kazi zifuatazo:
- Hueleza au kufafanua wazo maalum
- Kuwa na mawazo yaliyo katika mantiki
- Kuwa na mifano ya kutolea ufafanuzi.
Mkwaju (/)
Kutenga maneno mawili yenye maana sawa yanapotumika kwa pamoja. Mfano: mofimu ya njeo / wakati Hutumika kutenga namba za kumbukumbu na tarehe. Mfano: Kumb. 03/DA/20078 11/08/2014
Insha ni maandishi au masimulizi juu ya jambo au kitu fulani. Uandishi wa insha huwa katika aya.
MADHUMUNI YA UANDISHI WA INSHA
- Kujua ni jinsi gani mwandishi anaweza kujitegemea katika kuwaza na kujenga mawazo yake kwa makini.
- Kujua ni jinsi gani mwandishi anaweza kuandika mawazo yake kwa ufupi au kwa urefu kwa watu wengine.
MAMBO YA KUZINGATIA KATIKA UANDISHI WA INSHA
- Kuweka vidokezo vya msingi vinavyohusiana na habari uliyopewa.
- Kugawanya insha katika aya mbalimbali.
- Kuwa na mpangilio mzuri wa matumizi ya maneno.
- Kutumia lugha inayoeleweka.
- Mpangilio mzuri wa mawazo wenye kuzingatia mantiki.
- Kutokutumia lugha ya mkato
- Kutumia msamiati wa kutosha.
- Kuzingatia sarufi ya lugha
- Kuzingatia matumizi ya alama mbalimbali za uandishi.
- kuhakikisha insha inafuata na kujali matumizi ya nyakati mbalimbali.
- Insha lazima iwe na sehemu kuu tatu: Mwanzo, Kiini, Mwisho
Kuna aina nyingi za insha lakini zinaweza zikawekwa katika makundi makuu mawili:
- Insha za wasifu / kitawasifu
- Insha za hoja
NB: Baadhi ya wataalam huzigawa insha katika makundi makuu matatu.
- Insha za wasifu
- Insha za kisanaa
- Insha za hoja.
Nini maana ya insha za wasifu
Insha za wasifu ni insha ambazo huelezea sifa za kitu, hali au mtu fulani. Sifa zinaweza zikawa nzuri au mbaya.
Insha za Hoja
Hizi ni insha ambazo hutetea mawazo ya aina fulani na kupinga mengine kwa uthibitisho dhahiri.
Insha za kisanaa
Hizi ni insha ambazo hutumia vipengele mbalimbali vya kifasihi katika kuwasilisha ujumbe. Mbinu haze ni kama vile nahau, methali, misemo, tamadhali za semi na mbinu nyingine za kisanaa.
NB: Insha zisizo za kisanaa ni insha ambazo hazitumii lugha ya kifasihi katika kufikisha ujumbe wake.
Insha kwa kawaida hugawanyika katika sehemu kuu tatu ambazo ni:
- Utangulizi / Mwanzo wa insha
- Kiini cha insha / kati
- Mwisho wa insha / hitimisho
MWANZO WA INSHA (Utangulizi)
- Hutoa maelezo mafupi kuhusu mada ya insha.
- Ufafanuzi wa fasihi ya jambo linalozungumzwa.
- Uhusiano wa mada na vitu vingine vinavyohusiana nayo.
- Huonyesha muhtasari wa mambo yatakayozungumzwa kwenye insha.
- NB: Kwa kawaida utangulizi huwa na aya moja.
KIINI CHA INSHA
- Hii ndiyo sehemu kuu ya insha.
- Huonyesha mawazo makuu kuhusu mada inayojadiliwa.
- Mawazo hupangwa katika aya tofauti kwa mtiririko wa mantiki.
- Kila wazo kuu:
- Linafafanuliwa kwa kina.
- Linaambatana na mifano halisi.
- Lazingatia kichwa cha habari cha insha.
HITIMISHO
- Hutoa msisitizo wa hoja zilizoelezwa kwenye kiini.
- Huweza kutoa:
- Msimamo wa mwandishi.
- Maoni binafsi.
- Mapendekezo kuhusu jambo lililozungumzwa.
NB: Hitimisho mara nyingi huwa ni muhtasari wa yaliyosemwa kwenye insha.
Mwalimu
Unasoma somo hili? Niulize nikuelezee chochote kilichomo.
Ingia ili kumuuliza Mwalimu wa AI wa Sonza kuhusu mada hii.
Ingia ili kuuliza