Mada za sehemu hiiUtungajiMada 4
- insha
- Uandishi wa barua na kadi za mialiko
- Uandishi wa kazi za kifasihi
- Usimulizi ****
UTUNGAJI WA BARUA
Katika uandishi wa barua, mambo yafuatayo yazingatiwe:
- Barua za kirafiki
- Barua za kiofisi/kikazi
- Barua za simu
- Barua za mialiko
- Barua za magazeti
- Barua za kutoa taarifa
- Mifano iongezwe katika barua za kikazi na magazeti.
- Katika barua za mialiko mfano utolewe uonyeshwe.
- Utungaji wa matangazo mfano utolewe/uonyeshwe.
Hizi ni barua rasmi ambazo huandikwa kwa madhumuni mbalimbali kama vile kuomba kazi, kutuma na kupokea taarifa rasmi, kuomba nafasi ya kusoma, kuomba likizo, kuomba uhamisho.
Mambo ya kuzingatia
- Anuani ya mwandishi ambayo hukaa juu upande wa kulia.
- Tarehe inayokaa chini ya anuani ya mwandishi.
- Anuani moja au zaidi ya mwandishi inayokaa upande wa kushoto baada ya kumbukumbu namba.
- Salamu "Ndimi".
- Barua yenyewe ufafanuzi wa kusudio la barua.
- Mwisho wa barua.
- Sahihi ya mwandishi.
- Jina la mwandishi (kamili).
- Cheo cha mwandishi.
Mfano
MTAA WA MTAKUJA, S.L.P 14631, MAJENGO – MOSHI.
13/11/2012
MENEJA MKUU, KIWANDA CHA MATOFALI, S.L.P 87, MOSHI.
Ndugu,
YAH: OMBI LA KUJA KUJIFUNZA KUFYATUA MATOFALI
Kichwa cha habari hapo juu chahusika. Sisi ni kikundi cha vijana kumi na tano (15) ambao tumeamua kujiarijiri wenyewe kwa kufanya kazi ya kufyatua matofali.
Tunaomba kutembelea kiwanda chako kwa lengo la kujifunza zaidi.
Ni matumaini yetu kwamba ombi letu litakubaliwa.
Wako mtiifu,
…………………..
Vai Selis Chalamila (Katibu wa kikundi)
Hizi ni barua ambazo huandikwa na wasomaji mbalimbali wa magazeti na kupelekwa au kutumwa kwa mhariri wa gazeti husika.
Madhumuni
- Kupongeza kuhusu jambo fulani
- Kufichua maovu fulani
- Kutoa maoni/mapendekezo kuhusu jambo fulani
Mambo ya kuzingatia / Muundo
- Kuwa na kichwa cha barua ambacho huandikwa mwanzoni kwa herufi kubwa au kwa wino mzito.
- Mwanzo wa barua ambao huanza na "Ndugu Mhariri," Lazima kuwe na salamu.
- Barua yenyewe na huwa na ufafanuzi wa hoja kwa kutolewa katika sehemu hii.
- Mwisho wa barua mara nyingi huwa na maoni, maombi au mapendekezo.
- Jambo la mwisho ni jina la mwandishi, anwani, na tarehe. Hivi huandikwa chini ya barua upande wa kushoto.
Mfano
SHULE ZITUMIKE KUKUZA VIPAJI
Ndugu Mhariri,
Miaka ya nyuma swala la kukuza michezo shuleni lilikuwa linapatiwa kipaumbele. Hii ilidhihirishwa na kila shule kuwa na viwanja kwa ajili ya michezo mbalimbali.
Kwa miaka ya karibuni mambo siyo hivyo tena kwenye baadhi ya shule, viwanja hivyo vimeongezwa majengo kiasi kwamba sasa kunabakia sehemu finyu kwa ajili ya kufanya michezo hiyo. Wanapolazimika kufanya hivyo hutakiwa kwenda eneo la mbali, jambo ambalo linakuwa sio rahisi kulitekeleza mara nyingi.
Hata hivyo, kwa ushauri wangu naona kuwa shuleni ambapo wanafunzi bado ni wadogo wana nafasi nzuri ya kuendeleza vipaji vyao vya michezo.
Hii inawezekana sio kwa kusoma darasani bali kwa kufanya mazoezi ya michezo husika.
Tunaomba waalimu na mamlaka husika waliweke hilo maanani ili vijana waweze kweli kukuza vipaji vyao vya michezo. Ni kwa njia hiyo pekee ndiyo tutaweza kupata wanamuziki bora, wanariadha makini, waigizaji hodari wacheza mpira wa kiwango kinachoastahili na mabondia wa kiwango cha kimataifa. Hapo tunaweza tukawapata wakina Filbert Bayi wapya, wakina Abdallah Kibasen wapya, akina Mbaraka Mwishekhe wapya nk.
Fausta John, S.L.P 514, MOSHI
Ni barua ambayo kwa kawaida huandikwa kumualika mtu katika jambo fulani mfano harambee, sherehe, mkutano, semina, dhifa, warsha, kongamano.
Mambo ya kuzingatia
- Jina la mwandishi na anuani yake
- Jina la mwandikiwa/mwalikwa
- Lengo la mwalikaji kwa ufupi
- Tarehe ya mwaliko
- Mahali pa mwaliko
- Siku na wakati wa kukutana
- Mahali pa kupeleka jibu
Mfano wa barua rasmi
Bwana na bibi John wanayofuraha kukualika bibi Vai kwenye sherehe ya kumpongeza mtoto wao mpendwa Samweli kwa kumaliza darasa la saba, siku ya Jumapili tarehe 28/07/2013 kwenye ukumbi wa Uhuru Park Majengo saa kumi jioni.
Jibu kwa: Emerco Mashelle 0713 – 208123
Kumbuka: Wakati mwingine barua za mialiko huandikwa kama barua za kindugu ila huwa na maneno machache ili zisipoteze lengo maalumu.
Mfano wa barua ya kirafiki
Kijiji cha Kafule, S.L.P 15, Itumba – Mbeya
18/07/2013
Kwako mpendwa Vai,
Salam, Tarehe 11/08/2013 ninaadhimisha sikukuu ya kuzaliwa kwangu, nakualika ufike tufurahi pamoja kwenye Chakula kuanzia saa tano usiku nyumbani kwangu. Tafadhali naomba unijibu. Kufika kwako ndiyo furaha yangu.
Rafiki yako, Halima
Kumbuka: Kama barua ya mwaliko ni rasmi, yaani ya kiofisi, majina ya mwandikiwa huambatana na cheo chake. Mfano Profesa, Sheik, Mchungaji, Daktari n.k ambayo hutumika sambamba na maneno ndugu, bwana, na bibi. Wakati mwingine barua za mwaliko huandikwa katika karatasi maalum na kuitwa kadi za mwaliko.
Simu za maandishi ni njia mojawapo ya mawasiliano ya haraka miongoni mwa watu. Mtu anayeandika huipata haraka iwezekanayo kulingana na barua za kawaida. Barua za simu huwa ni fupi, lakini zenye ujumbe uliowazi na unaoeleweka. Ufupi wa barua za simu hutokana na gharama za malipo kwa sababu gharama za simu hulipiwa kulingana na idadi ya maneno yanayoandikwa.
Mambo ya kuzingatia
- Anuani ya anayepelekwa taarifa. Hii ni lazima iwe kamili na wazi ili kuziwezesha barua hiyo imfikie mlengwa bila ya matatizo yoyote.
- Taarifa au ujumbe. Hiki ndio kiini cha simu, ni vizuri kikaandikwa kwa ufupi na kueleweka, epuka kuandika mambo yasiyokuwa ya lazima.
- Jina la mwandishi. Ni vizuri kuandika kwa herufi kubwa kurahisisha usomaji.
- Barua ya simu huandikwa katika karatasi maalumu.
- Hakuna barua ya simu ambayo husafirishwa bila kulipiwa.
Mfano
ASHA MWANASEFU SLB 404060 MOSHI
FIKA HARAKA BABA ANAUMWA HAMISI
Hotuba ni maelezo ambayo hutolewa na mtu mbele ya hadhira ya watu kwa madhumuni mbalimbali kama vile kubainisha watu kufanya kazi, kutoa taarifa fulani, kufanya kampeni fulani n.k
Sifa za Hotuba
Hotuba yoyote nzuri ni lazima izingatie mambo yafuatayo:
- Ukweli wa habari na taarifa inayotolewa.
- Ufasaha wa lugha ili kuifanya hotuba iweze kupendeza na kueleweka vizuri.
- Nidhamu yaani kuwa na adabu njema unapohutubia na unapokuwa umesimama mbele ya watu.
- Mantiki nzuri yaani mfuatano mzuri wa mawazo na fikra.
- Sauti ya kusikika wazi pamoja na ishara zinazoeleweka iwapo hotuba inatolewa mbele ya watu.
Aina za Hotuba
- Mahubiri — Hizi ni hotuba zinazohusu mafundisho ya dini na hutolewa makanisani, misikitini, mbele ya waumini na pia kwa njia ya redio au televisheni.
- Hotuba za kisiasa na za kiserikali — Hizi ni hotuba zinazohusu mambo ya kiserikali na vyama vya siasa kwa lengo la kufafanua maazio au sheria, kampeni za kisiasa, kuhimiza watu kutenda jambo fulani n.k.
- Mihadhara au masomo ya darasani — Hizi ni hotuba au mafundisho yanayotolewa na waalimu shuleni hasa wanapokuwa wanafundisha kundi kubwa la wanafunzi hasa vyuo vikuu.
- Risala — Hii ni hotuba au taarifa fupi ambayo husomwa mbele ya kiongozi kwa niaba ya kundi fulani la watu ili kutoa maelezo au kuonesha msimamo wa kundi hilo kwa kiongozi husika.
Kumbuka: Baada ya kusomwa, kwa kawaida risala hiyo hukabidhiwa kwa mhusika katika maandishi kama kumbukumbu ya kudumu.
Muundo wa Hotuba
Kwa kawaida, hotuba huwa na muundo ufuatao:
-
Mwanzo Huu ni sehemu ya mwanzo ya hotuba ambayo huwa na salamu zinazotegemea hadhara iliyopo na lengo la hotuba. Salamu hizi hutumika kuwaheshimu wasikilizaji na kuonyesha heshima kwa mazingira ya tukio.
-
Utangulizi Sehemu hii hutumika kutambulisha mhutubiaji na hadhara iliyopo, kwa kuzingatia vyeo vyao. Mfano wa utambulisho ni: "Mheshimiwa Rais, Mheshimiwa Waziri Mkuu, Waheshimiwa Wabunge, Waheshimiwa Madiwani, Waheshimiwa Wakuu wa Shule, Waheshimiwa Waalimu, mabibi na mabwana." Katika utangulizi, kunaweza pia kuwa na shukrani na muhtasari wa hotuba itakayotolewa ili kutoa mwangaza wa ujumbe utakaozungumziwa.
-
Kiini cha Hotuba/Kati Hii ni sehemu muhimu zaidi ya hotuba ambapo mhutubiaji hutoa ujumbe kwa hadhira. Katika sehemu hii, mhutubiaji anatoa ufafanuzi na kueleza kwa kina yale yaliyomsukuma kutoa hotuba hiyo kwa hadhira husika. Huu ni wakati ambapo ujumbe mkuu wa hotuba unafikishwa kwa hadhira.
-
Mwisho Huu ni muhtasari wa yale yaliyoelezwa katika hotuba, ambapo mhutubiaji anajikita katika kumalizia ujumbe wake na kutoa muktadha wa lengo kuu la hotuba. Sehemu hii inaweza kuwa na hitimisho au wito kwa hatua zinazohitajika.
-
Risala Kamusi ya Kiswahili Sanifu (TUK: 1981) inafafanua risala kuwa ni taarifa inayopelekwa kwa mtu au watu fulani, mara nyingi ikiwa na lengo la kueleza hoja inayotakiwa. Risala ni hotuba fupi inayosomwa mbele ya kiongozi kwa niaba ya kundi fulani la watu ili kutoa maelezo au kuonyesha msimamo wa kundi hilo kwa kiongozi.
Risala huwa na sehemu kuu tatu:
- Mwanzo wa risala
- Kati au kiini cha risala
- Mwisho/hitimisho la risala
Mwanzo
Utangulizi wa risala, ambao unaweza kuhusisha:
- Salamu
- Ukaribisho wa wahusika
- Lengo kuu la risala
Kati/Kiini
- Sehemu muhimu zaidi ya risala.
- Hufafanua masuala mbalimbali, kama vile:
- Mafanikio yaliyopatikana
- Matatizo na changamoto zilizojitokeza
- Mapendekezo ya kifasihi au kwa vitendo
- Maombi ya kutatua changamoto au kuboresha hali iliyopo
Mwisho
- Msisitizo wa yale yaliyofafanuliwa kwenye kiini cha risala.
- Hutoa shukrani kwa wasikilizaji au wasomi.
- Hitimisho la risala.
Mambo ya kuzingatia
- Kichwa cha habari (huandikwa kwa herufi kubwa)
- Kutaja aina ya biashara au huduma zinazotakiwa na bei zake.
- Kutaja aina za bidhaa au huduma zinazotolewa na bei zake.
- Kutaja mahali inapotolewa huduma/bidhaa hizo yaani mji, mtaa, kijiji n.k
- Kutaja namna ya kuwasiliana
Mfano wa Tangazo
TANGAZO
Vitabu, Vitabu, Vitabu.
Wale wauzaji maarufu wa vitabu vya Injili/Dini wameleta Ingizo jipya. Fika dukani kwao Mtaa wa Malapa, Buguruni, Dsm.
Kwa mawasiliano zaidi; Piga simu zifuatazo; 0765459146
Mwalimu
Unasoma somo hili? Niulize nikuelezee chochote kilichomo.
Ingia ili kumuuliza Mwalimu wa AI wa Sonza kuhusu mada hii.
Ingia ili kuuliza