Kughani shairi kwa kuzingatia kanuni za mashairi, vina, mizani na kituo
Shairi mashairi ni tungo zenye kutumia mapigo ya silabi kwa utaratibu maalumu wa kimuziki kwa kutumia lugha ya mkato, lugha ya picha na tamathadi za semi.
- Mashairi ya kimapokeo
Haya ni mashairi yanayozingatia kanuni za urari (ulinganifu) wa mizani, vina, idadi ya mistari katika kila ubeti na kituo katika shairi. Vilevile haya huitwa mashairi funge
- Mashairi huru
Haya ni mashairi yasiyozingatia kanuni za kimapokeo yaani hayazingatii kanuni za urari (ulinganifu) wa mizani, vina, idadi ya mistari katika kila ubeti na kituo katika shairi, mashairi haya huitwa mashairi ya kisasa.
Vina ni silabi zenye sauti ya namna moja zinazotokea katikati au mwishoni mwa kila mshororo wa kila ubeti wa shairi. Hivyo shairi lina vina vya kati na vina vya mwisho. Hi shairi lako lihesabike kama limetimia vina ni lazima herufi za kati na herufi za mwisho za ubeti ziwe zinafanana.
Mfano:
Tulopeleka bungeni, wamegeuka nyang'au Mafisadi kama nini, baladhuli mabahau Wanavunja mpini, konde wamelisahau Zamani za siku hizi, mambo siyo yavyokua
Vina vya kati ni ni na vina vya mwisho ni u
Mizani ni ulinganifu wa idadi ya silabi katika kila kipande au mistari ya ubeti wa shairi. Mara nyingi mashairi ya kimapokeo huwa na mizani nane (8) kwa kila kipande na mizani kumi na sita (16) kwa kila mstari (mshororo)
Mfano:
Kiswahili ni kitamu, kuongea na kusoma Daima hakishi hamu, kama mtoto na mama Jifunze ukifahamu, ukizungumze vyema Kiswahili lugha yangu, sikuachi asilani
Huu ni mstari wa mwisho katika kila ubeti wa shairi, kituo pia huitwa kimalizio au kiini mara nyingi hujirudia rudia katika kila ubeti.
Mfano:
Yamezidi mitaani, madawa yo kuenea Si bangi si heroini, nani ametuletea Nipigapo darubini, vijana ndo meumia Nani alotuingiza, kwenye janga la kulevya
Afya zimezorota, miili medhoofika, Uraibu ni matata, ndoa kusambaratika, Mirungi wakishapata, watoto watairuka, Nani alotuingiza kwenye janga la kulevya.
Kweli inasikitisha, hali iliyotufikia, Serikali hakikisha, vituo mmeviweka, Madawa kuyapotosha, ukarabati kunyooka, Nani alotuingiza kwenye janga la kulevya
Joka lilokati yetu, mola tampa adhabu, Asambazae kwetu, wana wetu kuharibu Mali na cheo si kitu, ipo siku utajibu Nani alotuingiza kwenye janga la kulevya
Hivyo kituo ni; Nani alotuingiza kwenye janga la kulevya.
Mwalimu
Unasoma somo hili? Niulize nikuelezee chochote kilichomo.
Ingia ili kumuuliza Mwalimu wa AI wa Sonza kuhusu mada hii.
Ingia ili kuuliza