Mada za sehemu hiiKutafsiri Na KukalimaniMada 2
- Kutafsiri
- Kukalimani
Profesa Mwansako (1961) "Kitangulizi cha Tafsiri" anafasili tafsiri kuwa ni zoezi la uhawilishaji wa mawazo katika maandishi kutoka lugha moja kwenda nyingine. Pia TUKI toleo la pili (2004) inaeleza kuwa "Tafsiri ni maana ya maneno kutoka katika matini iliyoandikwa katika lugha moja kwenda lugha nyingine."
Tafsiri ni kubainisha maneno kutoka lugha asilia na kuyaweka katika lugha lengwa kwa maandishi bila kupoteza, kupotosha au kubadili maana. Kazi ya kutafsiri hujihusisha zaidi na maandishi.
Kuna aina nyingi zinazotumiwa katika kazi ya kutafsiri:
- Tafsiri ya neno kwa neno
- Tafsiri ya sisisi
- Tafsiri ya kisemantiki
- Tafsiri ya kimawasiliano
Ni tafsiri ambayo huzingatia maana iliyotolewa na mwandishi wa lugha asilia na hairuhusiwi kufanya marekebisho katika lugha asilia ili kukidhi matakwa ya lugha lengwa. Mtafsiri anatakiwa kutafsiri kila kipengele katika matini ya lugha asilia ili kupata maana iliyokusudiwa katika lugha asilia kwa kufuata sarufi ya lugha lengwa.
Mfano: CHANZI: Mwalimu Juma alimaliza shule ya msingi mwaka 1982 na alijiunga na shule ya Sekondari Mzumbe 1983.
LENGWA: Juma the teacher completed his Primary school Education in 1982 and joined Mzumbe Secondary School in 1983.
Ubora
Ina uwezo mkubwa wa kuendeleza lugha lengwa kwa kuingiza miundo na misemo kutoka lugha asilia.
Mfano: CHANZI: Wasalimie wote nyumbani
LENGWA
Kusaidia katika kunukuu maneno ya mtu mwingine kwani kila neno hutakiwa litafsiriwe jinsi lilivyo pasipo kupoteza maana hata kipengele kimoja.
Udhaifu
Tafsiri ya kisemantiki hautilii maanani nahau na misemo maalum inayohusiana na utamaduni wa lugha lengwa.
Mfano: CHANZI (Kiingereza) Anna married John.
LENGWA (Kiswahili) Anna amemuoa John
Hii ni tafsiri ambayo huwa inazingatia hadhara ya matini ya lugha lengwa kwa kumjali sana msomaji wa matini hiyo. Hii ni tafsiri huru inayompa ubavu mfasiri kuongea au kupunguza maneno ya matini ya lugha asilia wakati wa kufasili. Jambo la kuzingatia ni kwamba ujumbe uwafikie walengwa kwa namna ile ile bila kupoteza wazo la matini ya lugha asilia. Mfasiri anauhuru wa kutumia maneno yanayolingana na misemo, methali, nahau, utamaduni na mazingira ya lugha lengwa.
Ubora
Njia hii hufuata kanuni, taratibu na sheria za lugha lengwa kwa kuzingatia mwelekeo wa utamaduni wake, historia, mazingira na hadhira lengwa.
Mfano: CHANZI (Kiingereza): Anna married John.
LENGWA (Kiswahili): John amemuoa Anna.
Tafsiri ya kimawasiliano husaidia hadhira lengwa kuelewa kwa urahisi. Tafsiri hii ni rahisi kwa kuwa uhusisha kile wanachosoma na hali halisi katika mazingira yao.
Tafsiri hii uhusu mabadiliko kulingana na historia, itikadi na mazingira ya hadhira ya lugha lengwa.
Huweza kuboresha au kusahihisha kifikiriwacho kuwa kilipotoshwa na matini ya lugha asilia ili kiweze kueleweka vizuri katika matini ya lugha lengwa.
Udhaifu
Haina uwezo wa kuendeleza, kuingiza miundo au misemo kutoka katika lugha asili kwenda lugha lengwa kwa sababu haizingatii wazo la jumla la kiutamaduni kwa lugha lengwa.
Kitendo cha mfasiri kuegemea sana kwenye mawazo, historia, utamaduni, mazingira na itikadi ya lugha lengwa inaweza kupotosha.
Mfano: Wakati wa ugomvi wa Marekani na Iraq vyombo vya habari vya Iraq vilimuita Rais Sadam Hussein Mheshimiwa. Sentensi hizo hizi zilitafsiriwa na vyombo vya habari ya Marekani kuwa "Gaidi Rais Saadam Hussein".
Hii ni tafsiri ambayo mofimu na maneno hufasiliwa yakiwa pwekepweke kwa kuzingatia maana zake za msingi bila kujali muktadha. Mpangilio wa mofimu na maneno wa lugha chanzi hubakia vilevile. Maneno yanayofunga maana na utamaduni hufasiriwa kisisisi. Matini ya tafsiri yaani matini ya lugha lengwa huandikwa chini ya matini chanzi.
Mfano: CHANZI: Alikwenda mpaka nyumbani kwake.
LENGWA: He/ passed /go/until/at/house/his
Ubora
Husaidia kuelewa jinsi lugha chanzi inavyofanya kazi na jinsi muundo na maumbo yake yalivyo.
Husaidia katika kuainisha muundo na maumbo ya semi za lugha ngeni zinazofanyiwa uchunguzi
Udhaifu
Tafsiri hii haitoi kwa uwazi maana inayokusudiwa kwa sababu nahau na misemo inayohusiana na utamaduni hufasiriwa kisisisi.
Ni aina ya tafsiri ambayo maneno hufasiriwa ya kuwa pwekepweke kwa kuzingatia maana zake za msingi katika lugha chanzi bila kujali sana muktadha. Lakini hufasiriwa kufuatana na mfumo wa kisarufi, hususani sintaksia ya lugha lengwa.
Mfano: CHANZI: He was taken to the central police station
LENGWA: Alipelekwa kituo cha kati cha polisi
(Neno "kituo cha kati cha polisi" limetumika badala ya kituo kikuu cha polisi)
Kwa ujumla mfasiri kabla ya kufanya mchakato wa kutafsiri anapaswa kuainisha matini kabla ya kuanza hatua ya kwanza ambayo ni maandalizi, kuainisha matini ni kitendo cha kuzigawa matini katika aina mbalimbali kutokana na mahitaji yanayotofautiana ya kifasiri kwa kila aina ya matini. Uainishaji huu wa matini hujikita katika mikabala mitatu:
- Matini zinaweza kuainishwa kwa kufuata matumizi ya istilahi katika matini.
- Kwa kufuata mada
- Kwa kufuata dhima kuu za lugha
- Maandalizi: Humuhitaji mfasiri kufahamu vizuri maudhui ya matini chanzi. Mfasiri huisoma matini nzima ya lugha chanzi ili kubaini ujumbe, mtindo na kuweka alama maalumu sehemu zenye utata au ugumu. Pia mfasiri hubaini utamaduni wa mwandishi wa wasomaji wa matini chanzi
- Uchambuzi: Mfasiri huchunguza maneno pamoja na maelezo muhimu ya matini chanzi yaliyoandikwa katika hatua ya maandalizi. Zoezi hili hufanywa kwa kutumia maendeleo mbalimbali kama vile kamusi na istihadi za vitabu mbalimbali.
- Kuhamisha matini chanzi kwenda matini lengwa: (Uhamishaji) Mfasiri huhamisha mawazo, maana na ujumbe kutoka matini asilia kwenda matini lengwa. Mfasiri hufanya maamuzi juu ya zana za kisarufi zinaweza kutumiwa katika matini lengwa zitakazoelezea maana za matini asilia kwa usahihi zaidi.
- Tafsiri: Mfasiri hupata nafasi ya kufanya marekebisho kwa kuzingatia umbo la matini lengwa na kila lengo asilia.
- Udhalisuwa rasimu ya kwanza: Katika hatua hii, mfasiri anapata nafasi ya kwanza ya kusahihisha matini iliyokwisha tafsiriwa. Mfasiri anapaswa aisome rasimu nzima kwa sauti kwa kuzingatia mambo yafuatayo:
- Kusahihisha makosa ya kisarufi na miundo ya tungo isiyoeleweka vizuri.
- Kunyoosha sehemu zenye tafsiri ya mzunguko na zenye matumizi ya visa yasiyo ya lazima
- Kurekebisha sehemu zenye miunganisho inayozuia mtiririko mzuri wa matini.
- Kubaini iwapo mada au ujumbe mkuu wa matini unajitosheleza waziwazi katika tafsiri.
- Kuona kuwa lugha inayotumika ina uasili unaokubalika kulingana na mada na umbo la matini lengwa.
- Kubaini iwapo lugha inayotumika inazingatia utamaduni wa hadhira lengwa.
- Kusomwa kwa rasimu ya kwanza na mtu mwingine. Mfasiri humpatia mtu mwingine matini lengwa ili aisome kuona kama inaeleweka na ina mtiririko mzuri wa mawazo. Dhima ya msomaji wa pili ni kuona kama tafsiri ipo sahihi, inaeleweka na ina mtiririko mzuri unaokubalika. Pia msomaji wa pili hutoa mapendekezo ya marekebisho yanayohitajika.
- Usawidi wa rasimu ya mwisho. Mfasiri akishapata maoni ya msomaji wa pili, huyatunza maoni hayo kusahihisha tena rasimu yake na hatimaye hutoa rasimu ya mwisho. Hii ndiyo itakuwa matini lengwa
Mwalimu
Unasoma somo hili? Niulize nikuelezee chochote kilichomo.
Ingia ili kumuuliza Mwalimu wa AI wa Sonza kuhusu mada hii.
Ingia ili kuuliza