Mada za sehemu hiiKutafsiri Na KukalimaniMada 2
- Kutafsiri
- Kukalimani
Tuki (2004) anasema "Mkalimani ni mtu anayefasiri mazungumzo papo kwa papo kutoka lugha nyingne kwenda nyingine". Hivyo twaweza sema ukalimani ni kitendo cha kuhamisha maneno kutoka lugha moja kwenda nyingine kwa kuongea au mazungumzo. Katika ukalimani mawazo au jambo lazima liwe katika mazungumzo na sio maandishi.
- Ukalimani wa papo kwa papo, mkalimani anatafsiri papo kwa papo kutoka lugha chanzo kwenda lugha lengwa. Mfano: katika mikutano ya kidini, mihadhara n.k.
- Ukalimani wa maandalizi, hapa mkalimani na mtoa mada hukaa pamoja na kuongea nini cha kufanya. Mfano: vuto za kisiasa, mkalimani hukaa na mtoa hotuba ili kuwekeana mpaka katika kuongea.
- Ufasaha na usanifu wa lugha
- Mpangilio mzuri wa wazo
- Ukweli na uwazi katika kujieleza
- Kuwa msikivu, mtulivu
- Aweze kuweka akili yake kwa yale yanayozungumzwa / Aweze kufahamu yanayozungumzwa
- Umakini, ili aweze kufasiri kinachozungumzwa
- Kujua matamshi ya mzungumzaji
- Kuwa makini na kile kinachozungumzwa
- Awe mtu anayezielewa lugha chanzo na lugha lengwa vizuri.
- Awe ni mtu ambaye pande zote za lugha anazozikalimani ili kuelewa mila na desturi za watumiaji wa lugha hizo.
- Awe standi wa ukalimani, hapa anatakiwa awe hodari wa kukalimani, kuzungumza vizuri maneno kushaide awe na uwezo wa kukalimani neno kwa neno au sentensi kwa sentensi.
- Muadrifu ambaye awezi kupotosha au kubadili maana ya kinachozungumzwa.
- Asiwe mbaguzi, hii ina maana asibague kijinsia, dini, umri au kisiasa bali afikishe kinachokusudiwa.
- Awe makini kusikiliza kinachozungumzwa ili kutokanchanganya maana ya ujumbe unaokusudiwa kuifikia jamii.
- Msamiati wa lugha lengwa hukua, mfano baadhi ya maneno ya lugha ya kigeni hukua Uchukuliwa na kuwekwa katika lugha lengwa.
- Kupanua uelewa wa kufahamu mambo kwa msomaji na msikilizaji.
- Kukua na kuenea kwa tamaduni mbalimbali. Mfano: baadhi ya tamaduni za kigeni zimeingia katika Tanzania na pia tamaduni za kitanzania zimesambaa duniani.
- Husaidia kupashana habari, kuwasiliana. Mfano: wasioelewa lugha ya kigeni huweza kupata habari kupitia kufasiriwa.
- Masuala ya itikadi na uelekeo, kutofautiana katika itikadi kunaweza sababisha kutoeleweka. Mfano: Kingereza, Iraq walitangaza "Honourable President Sadam Hussein." Marekani walitangaza "Gaidi Raisi Sadam Hussein."
- Tofauti za kimazingira. Mfano:
| Kiingereza | Kiswahili |
|---|---|
| Autumn | Vuli |
| Winter | Kipupwe |
| Summer | Kiangazi |
- Tofauti za misemo, nahau na methali.
Kupuuzwa kwa ukalimani na tafsiri hapa Tanzania hivyo kupelekea kukosa wakalimani mahiri.
Mwalimu
Unasoma somo hili? Niulize nikuelezee chochote kilichomo.
Ingia ili kumuuliza Mwalimu wa AI wa Sonza kuhusu mada hii.
Ingia ili kuuliza