Mada za sehemu hiiKuonesha Uelewa Wa Jambo Ulilolisikiliza Au KulisomaMada 2
- Kusikiliza na Kuonesha Uelewa wa jambo Alilosikilia
- Kusoma kwa Ufasaha na Kuonesha Uelewa Wa matini Aliyosoma
Kusikiliza na kuonesha uelewa wa maneno mbalimbali
1. Vitendawili
Kusikiliza na kutegua vitendawili
-
Kitendawili: Popoo mbili zavuka mto Jibu: Macho
-
Kitendawili: Naapa hivi sitarudi tena kwa mjomba Jibu: Majani
-
Kitendawili: Shamba langu kubwa lakini navunia kiganjani tu Jibu: Ndevu
-
Kitendawili: Tega nikutege Jibu: Mwiba
-
Kitendawili: Kila ninakoenda hunifuata Jibu: Kivuli
-
Kitendawili: Babu kajenga nyumba lakini haina mlango Jibu: Yai
-
Kitendawili: Kaa kule nami nikae huku turushe mawe pangoni Jibu: Kula ugali
-
Kitendawili: Babu kalala ndani lakini kasahau ndevu nje Jibu: Mhindi
-
Kitendawili: Kuku wetu hutagia miibani Jibu: Nanasi
-
Kitendawili: Kulia kwake ni kicheko kwetu Jibu: Mvua
2. Nahau
Kueleza maana ya nahau zifuatazo
-
Nahau: Kujikaza kisabuni Maana: kutia bidii
-
Nahau: Kula bata Maana: Kula raha
-
Nahau: Kuwa macho Maana: Kuwa mwangalifu
-
Nahau: Sinahali Maana: Ni fukara
-
Nahau: Kufa kishujaa Maana: Kufa lava kupigania haki
-
Nahau: Piga kithembe Maana: Kushindwa kutamka maneno
-
Nahau: Piga mbiu Maana: Toa tangazo kwa maneno
-
Nahau: Unga mkono Maana: Kukubaliana jambo
Mwalimu
Unasoma somo hili? Niulize nikuelezee chochote kilichomo.
Ingia ili kumuuliza Mwalimu wa AI wa Sonza kuhusu mada hii.
Ingia ili kuuliza