Mada za sehemu hiiUandishi Wa InshaMada 1
- Insha za wasifu
Taratibu za Uandishi
Alama na mpangilio wa maneno ni mojawapo ya vigezo vya kutambulisha mwandishi bora hodari kaziiwezekuwa nzuri inayoeleweka na wasomaji, mwandishi hana budi kutumia mfumo wa alama ili kumsaidia msomaji wapi pa kumpumzisha, kuuliza swali n.k baadhiya alama zifuatazo hutumika katika uandishi.
Mkato (,)
Alama hii hutumika:
- kuweka pumziko fupi katika sentensi
- kutenga maneno yaliyo katika orodha
- huonyesha sehemu mbili za sentensi zilizo kinyume
Mfano: Umoja ni nguvu, utengano ni dhaifu
Nukta (.)
Alama hii hutumika:
- kukamilisha sentensi
- kuonyesha ufupisho wa maneno
Mfano: R.T.D (Radio Tanzania Dar es Salaam)
Nukta Mkato (;)
Alama hii hutumika Kuunga sentensi mbili zinazoweza kusimama zenyewe bila kutumia kiunganishi.
Mfano: Hapo zamani za kale wazee walijiheshimi; sikuhizi hawajiheshimu. Humpa msomaji pumziko fupi katika sentensi.
Nukta/Pukta Pacha (:)
Alama hii hutumika kuunga sentensi mbili zinazoweza kusema zenyewe, bila kutumia kiunganishi
- kuunga/kuonesha vitu vilivyo katika orodha
Mfano: Nilileta vitu hivi: wino, karatasi, embe, ndizi na nanasi.
Alama ya Mshangao (!)
- Hutumika baada ya neno au usemi wa kushangaza au kushtuka
- Hutumika kuonesha msisitizo, kushangaa, kero n.k.
Mfano: Hivi ni kweli! Mwone alivyo.
Alama ya Kuuliza (?)
Huonesha hali ya kuuliza swali katika tungo/sentensi
Mfano:
- Wanakuja saa ngapi?
- Wanamaana gani?
Mabano [ ( ) ]
Hutumika kuonesha maana ya ziada katika sentensi
Mfano: Nchi yangu (Tanzania) naipenda sana
Kistari (-)
Hutumika kuunda maneno
Mfano: Ed-elfitr, Dar-es-salaam
Hutumika badala ya nukta mbili
Mfano: tulipofika mbugani – tuliwaona swala wamelala – Swala dume na watoto watatu.
- Hutumika kuonesha kama neno limekatwa kwa kuwa limefika ukingoni.
Alama za Mtajo (" ")
Hutumika kuonesha maneno yaliyosemwa na mtu mwingine katika sentensi.
Mfano: Nguchiro alisema "hakika mzee Ngwale ni katili sana"
Hutumika kubainisha maneno ya kigeni katika lugha nyingine.
Mfano: ("yes") katika Kiswahili.
Insha ni kifungu cha habari chenye kueleza hoja au picha za mtu juu ya jambo fulani.
Insha hugawanywa katika vifungu, navyo ni:-
Insha huweza kuwa na haya moja au wakili na kila haya hubeba wazo kuu moja.
Kuna aina kuu mbili za insha:
- Insha za wasifu
- Insha za hoja
| Insha za Wasifu | Insha za Hoja |
|---|---|
| Insha za kisanaa | Insha za kisanaa |
| Insha zisizo za kisanaa | Insha zisizo za kisanaa |
Insha za Hoja
- Hueleza mawazo fulani na hupanga mengine
- Mifano ya vichwa vya insha vifuatavyo ni vya insha ya hoja:
- Elimu itolewe kwa watoto wa kiume tu.
- Shule za kutwa ni bora kuliko shule za bweni.
Insha za Wasifu
Hii hueleza sifa za watu au vitu kama wanyama, milima, miti au mahali fulani.
-
Kichwa cha Insha Huandikwa kwa herufi kubwa katikati juu ya insha. Huandikwa kwa ufasaha na kwa muhtasari. Kichwa kisizidi maneno matano (5).
-
Mwanzo wa Insha Huzingatia tafsiri ya jambo linalozungumzwa, uhusiano wake na vitu vingine. Kwa kawaida mwanzo huzidi aya moja.
-
Kiini cha Insha Hii ni sehemu kuu ya insha huzingatia mawazo makuu ambayo hupangwa katika haya zenye mtiririko mzuri wa mawazo. Hueleza kwa undani juu ya jambo linalozungumzwa kwa uthibitisho.
-
Mwisho wa Insha Hutoa msisitizo kwa yaliyojadiliwa. Huonesha muhtasari wa yaliyojadiliwa na kuandikwa pamoja na hitimisho.
- Kichwa cha habari chenye kueleweka
- Kuandika kwa kufuata kanuni na taratibu za uandishi
- Kutumia lugha fasaha na rahisi.
- Andika mwisho wa insha unaowavutia wasomaji au wasikilizaji.
Misitu
Mimi naitwa Ajazi Mohamed natokea kijiji cha Njoro kilichopo Moshi mkoani Kilimanjaro. Katika kijiji hicho naishi na babu pamoja na bibi alikadhalika na ndugu zangu. Kila ifikapo jumamosi mimi na ndugu zangu huwa tunakwenda kukata kuni pia kuchuma matunda kama mananasi, maembe, machungwa pia maparachichi. Misitu husaidia kwa ajili ya kivuli, mvua pamoja na kuni. Pia misitu hiyo hiyo hutoa mbao kwa ajili ya kutengenezea vifaa vya nyumbani vikiwemo, meza, viti, makabati pamoja na vitanda. Pia mbao hutumika kujenga mapaa ya nyumba na kadhalika. Misitu hiyohiyo hupenda kukaa wanyama wakali kama vile mbwa mwitu, nyoka na wadudu wenye sumu wakiwemo nyuki, dondola. Misitu ipo sehemu mbalimbali ikiwemo Moshi, Arusha, Songea pamoja na Singida. Misitu ni hatari sana hasa kwa watoto wadogo kwenda peke yao msituni au mwanamke kutembea peke yake jioni au usiku huwa ni hatari sana kwa sababu msituni kuna wanyama wakali sana na unaweza kukutana na majambazi. Misitu ni muhimu kwa ajili ya mahitaji yetu ya nchi na ya nyumbani kwa ujumla pia tunasisitiza kutunza misitu, mazingira na maeneo tunayoishi.
Insha za Kisanaa
- Hutumia mbinu za kifasihi kama:
- Methali (mf. "Penye nia pana njia")
- Tamathali za semi (mf. sitiari, tashbihi)
- Misemo na nahau
- Lugha yake hupambwa ili kuvutia na kuibua hisia.
- Mfano: Insha ya kusimulia au kuelezea kwa mbinu za kuvutia.
Insha Zisizo za Kisanaa
- Hueleza moja kwa moja bila kutumia mbinu za kifasihi.
- Lugha yake huwa ya kawaida, rahisi na ya moja kwa moja.
- Lengo lake ni kueleza au kufundisha.
- Mfano: Insha yako ya "Misitu" ni ya aina hii.
Mwalimu
Unasoma somo hili? Niulize nikuelezee chochote kilichomo.
Ingia ili kumuuliza Mwalimu wa AI wa Sonza kuhusu mada hii.
Ingia ili kuuliza