Mada za sehemu hiiFasihi Kwa UjumlaMada 6
AINA ZA FASIHI
Kuna aina mbili (2) za fasihi
- Fasihi andishi
- Fasihi simulizi
i. FASIHI SIMULIZI
Ni fasihi ambayo hutumia masimulizi ya mdomo kufikisha ujumbe wake kwa jamii. Ni fasihi ambayo ni kongwe na ilianza tangu binadamu alipoanza kuishi duniani.
FASIHI SIMULIZI INA TANZU NNE NAZO NI
- Hadithi
- Semi
- Ushairi
- Maigizo
ii. FASIHI ANDISHI
Ni fasihi ambayo hutumia maandishi ili kufikisha ujumbe kwa jamii
Fasihi andishi ina tanzu nne
- Tamthilia
- Ushairi
- Ngonjera
- Riwaya
TOFAUTI KATI YA FASIHI SIMULIZI NA FASIHI ANDISHI
| NA | FASIHI SIMULIZI | FASIHI ANDISHI |
|---|---|---|
| i | Huwasilishwa na fanani kwa njia ya masimulizi au mdomo | Huwasilishwa kwa maandishi kwa njia ya maandishi |
| ii | Huifadhiwa kichwani na kusambazwa na mdomo au mazungumzo | Huifadhiwa kwa maandishi na kusambazwa kwa maandishi |
| iii | Huruhusu mabadiliko ya papo kwa papo | Hairuhusu mabadiliko ya papohapo kazi ikishaandikwa haibadiliki hadi toleo jingine |
| iv | Ina tanzu nne kama vile Hadithi, Semi, Ushairi na Maigizo | Ina tanzu nne kama vile Tamthilia, Ushairi, Ngonjera na Riwaya |
| v | Hadhira yake ni watu wale katika jamii, watoto, wazee na wasomi | Hadhira yake ni watu wale wanaojua kusoma na kuandika |
| vi | Ina umri mkubwa | Ina umri mdogo, imekuwepo baada ya ugunduzi wa maandishi |
| vii | Ni rahisi kusahau baadhi ya vipengele | Si rahisi kusahauliwa baadhi ya vipengele kwani imehifadhiwa kwa maandishi |
| viii | Muundo wake ni wa moja kwa moja | Mara nyingi muundo wake ni wa mchangamano unaruhusu urejeshi |
| ix | Huenda na wakati na mabadiliko ya matukio katika jamii | Haiendi na wakati kwa sababu ikishaandikwa haiwezi kubadilishwa |
Mwalimu
Unasoma somo hili? Niulize nikuelezee chochote kilichomo.
Ingia ili kumuuliza Mwalimu wa AI wa Sonza kuhusu mada hii.
Ingia ili kuuliza